HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 8, 2021

Waziri Lukuvi aipongeza NHC kwa ubunifu wa nyumba za gharama nafuu

 

*Wananchi baada kulipa kupitia mkopo wa Benki kumiliki nyumba ndani ya siku moja.

Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Makazi William Lukuvi amefurahishwa na ubunifu wa ujenzi wa nyumba bora na gharama nafuu unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambao umeanza kwa awamu hii ambapo wameanza kujenga nyumba 400 mkoani Dodoma.

Akizungumza mara baada ya kutembelea banda la NHC kwenye Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam Waziri Lukuvi amesema kwa mara ya kwanza ubunifu huo utawezesha mkopaji kupata mkopo na kupata nyumba kwa siku moja na shirika la Nyumba wamewawezesha wananchi mkopo ambao utakuwa chini ya asilimia 10.

Amesema kuwa awali miradi ya Ujenzi ilikuwa inafanywa wakiwa watu wamelipa na kuanza kusubiri nyumba huku wakiendelea kulipa fedha za kwa nyumba waluzopanga.

Waziri Lukuvi amesema kazi ya NHC imeanza kuonekana katika kuwanufaisha wananchi nyumba za gharama nafuu.

"Mwananchi atapewa mkopo benki atalipa Shirika la Nyumba na Shirika litampa ufunguo wa nyumba na hati ya kumiliki kiwanja kwa siku moja". Amesema Waziri Lukuvi.

Amewataka wananchi kuzichangamkia nyumba zinazojengwa na NHC ambazo zipo mkoani Dodoma ambazo Agasti Mwaka huu watazitoa kwa wananchi kwa utaratibu maalumu.

"Tunataka tuwaelekeze Real Estate Developers kama Shirika la Nyumba ndio mjenzi kiongozi, kama kiongozi tunataka kutoa masomo mawili kwanza, kila mwananchi anaeahidiwa au anaelipa kwaajili ya kupata nyumba lazima apate nyumba mara baada ya kulipia badala ya utaratibu wa sasa mtu anatoa Fedha ya kununua nyumba alafu hizohizo fedha zinatumika kufanya ujenzi na mwananchi kuanza anadanganywa anapewa nyumba baada ya miaka miwili au mitatu". Amesema Lukuvi.Waziri Lukuvi aipongeza NHC kwa ubunifu wa nyumba za gharama nafuu.
Waziri wa Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza mara baada ya kutembelea Banda la Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) katika maonesho ya 45 ya Biashara Kimataifa yanyoendelea kufanyika  viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Sabasaba jijini Dar es Salaam yanayoendela
Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akiangalia ramani ya mradi wa Nyumba zilizojengwa Dodoma kwa ajili ya wananchi zenye gharama nafuu wakaiti alipotembelea maonesho ya Sabasaba katika Banda la NHC.

1 comment:

  1. Awesome and interesting article. Great things you've always shared with us. Thanks. Just continue composing this type of post.

    ReplyDelete

Post Bottom Ad