HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 29, 2021

IGP SIRRO WANANCHI MSIDANGANYWE KUHUSU CHANJO YA UVIKO-19

 

 

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, amewataka Wananchi na Watanzania kwa ujumla wasidanganywe na watu wa chache au kikundi cha watu wanaowahamasisha kwa njia mbalimbali ikiwemo mitandao ya kijamii kuto kuchanjwa chanjo ya Uviko-19 ambapo zoezi la uchanjwaji wa chanjo hiyo lilizinduliwa jana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Dar es salaam.

IGP Sirro amesema hayo leo wakati wakiandikishiana hati ya makubaliano kati ya Shirika la Bima la Taifa na Jeshi la Polisi kupitia Shirika lake la Uzalishajimali ambapo shirika hilo litaweza kuwa wakala wa bima za maisha na ajali kwa watendaji wa Jeshi hilo la Polisi pamoja na familia zao huku Jeshi hilo likitoa ahadi ya kutanua wigo ili bima hiyo ya maisha iweze kuwafikia hata waendesha pikipiki maarufu bodaboda.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa Dkt. Elirehema Joshua amesema kuwa licha ya kuwepo kwa idadi ndogo ya wananchi wenye ufahamu wa masuala ya bima za maisha, ajali na mali ambapo kupitia shirika la uzalishajimali la Jeshi la Polisi litakuwa na wigo mpana wa kuwafikia wananchi pamoja na kuwezesha Watanzania wote kupata elimu na huduma zote za bima zinazopatikana nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad