Na Mwandishi Wetu, Kilosa
WAKATI
huu ambapo dunia inakabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, ipo
haja dhana ya utunzaji shirikishi wa vyanzo vya maji ikapewa kipaumbele
ili kuokoa rasilimali hiyo muhimu kwa maisha ya binadamu.
Kauli
hiyo imetolewa hivi karibuni na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya
Kilosa, Cheyo Nkelege wakati wa uzinduzi wa Ofisi ya Jumuiya ya Watumia
Maji katika Kijiji cha Msowero, ambapo ujenzi wake umesimamiwa na Bodi
ya Maji Bonde la Wami Ruvu.
Aidha, sambamba na mabadiliko ya
tabianchi yanayotajwa kuhatarisha uhai wa rasilimali maji, changamoto
nyingine inayotajwa ni ongezeko la shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo
hivyo, zinazosababisha hali ya uchafuzi wa mazingira.
Kwa upande
wake Makamu Mwenyekiti Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu, Norah Mambya
ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvi,
alisema dhamira ya ujenzi wa ofisi ya Jumuiya ya watumaji maji katika
eneo hilo utasidia ulinzi na uhifadhi endelevu wa rasilimali maji.
Kwa
upande wao baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Msowero, wameelezea namna
Jumuiya za Watumia maji zinavyosaidia kutunza na kulinda vyanzo vya maji
katika eneo hilo.
Katika hatua nyingine, imeelezwa kuwa mradi wa
ujenzi wa Ofisi ya Jumuiya ya Watumia Maji Katika Bonde Dogo la
TAMI/MSOWERO wilayani Kilosa hadi kukamilika umegharimu kiasi cha
Shilingi Milioni 72.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kilosa, Cheyo Nkelege, akikata utepe
kwenye Jiwe la Msingi kuashiria Ufunguzi rasmi wa Ofisi za Jumuiya ya
Watumia Maji katik Bonde dogo la Tami/ Msowero Wilayani Kilosa mkoa wa
Morogoro.
Kaimu
Mkurugenzi Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu, Elibariki Mmasi (Kulia)
akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kilosa, Cheyo
Nkelege wakati wa uzinduzi wa Ofisi ya Jumuiya ya Watumia Maji katika
Kijiji cha TAMI/MSOWERO, ambapo ujenzi wa Ofisi hiyo umesimamiwa na Bodi
ya Maji Bonde la Wami Ruvu.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kilosa, Cheyo Nkelege, akizungumza
na Wananchi wa Kijiji cha Msowero wakati wa Uzinduzi rasmi wa Ofisi ya
Jumuiya ya Watumia Maji katika Bonde dogo la Tami/Msowero Wilayani
Kilosa mkoa wa Morogoro.
Mkurugenzi
wa Rasilimali za Maji kutoka Wizara ya Maji Bi Praxeda Paul,
akizungumza wakati wa Uzinduzi huo, Waliokaa Meza Kuu Kutoka Kushoto ni
Kaimu Mkurugenzi Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu, (Kati) ni Kaimu
mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kilosa Cheyo Nkelege ( wa tatu Kushoto) ni
Bi Norah Mambya ambae ni Makamu Mwenyekiti Bodi ya Maji Bonde la Wamu
Ruvu.


Baadhi
ya Watumishi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu wakifuatilia tukio la
Uzinduzi rasmi wa Ofisi za Jumuiya ya Watumia Maji katika Bonde dogo la
Tami/Msowero wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro.


Kaimu
Mkurugenzi Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu Elibariki Mmasi akimuonesha
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kilosa Cheyo Nkelege maeneo
mbalimbali ya Ofisi za Jumuiya ya Watumia maji katika Bonde dogo la
Tami/ Msowero Wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro.
Watumishi
wa Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu wakiwa katika Picha ya Pamoja na
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kilosa, mara Baada ya kukamilisha
kwa hafla ya Uzinduzi wa Ofisi za Jumuiya ya Watumia maji katika Bonde
dogo la Tami/Msowero Wilayani Kilosa.

Wana
Jumuiya ya Watumia maji katika Bonde dogo la Tami/Msowero wakiwa katika
picha ya pamoja na Viongozi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami Ruvu,mara
Baada ya kukamilika kwa hafla ya Uzinduzi wa Ofisi za Jumuiya hiyo
katika Kijiji cha Msowero Wilayani Kilosa.
No comments:
Post a Comment