HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 21, 2021

TIMU 123 ZARINDIMA MBUNGE CUP WILAYANI LUDEWA

 


Na Shukrani Kawogo, Njombe.

Timu 123 za mpira wa miguu wilayani Ludewa mkoani Njombe zimejitokeza kushiriki ligi ya mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga iliyozinduliwa hivi karubuni na kushirikisha kata zote 26 wilayani humo.

Akizungumzia mashindano hayo mmoja wa wasimamizi wa ligi hiyo kutoka Katika chama cha mpira wa miguu wilayani humo Jimmy Haule amesema mashindano hayo yameanza vyema ambapo timu hizo ni kutoka katika vijiji vyote 77 vya wilaya hiyo ambazo zinashiriki mashindano hayo.

Amesema kwa sasa mashindano hayo yameanza katika hatua za makundi za vijiji ambapo timu itayopata ushindi itaingia katika mchuano ngazi ya kata kisha tarafa na hatimaye wilaya.

Amesema kuna baadhi ya kata mashindano hayo yamekuwa yakisimamiwa na watendaji kata ambao wamekuwa wakiwasiliana nao kwa ukaribu ili kujua endapo kuna changamoto zozote zinazojitokeza.

Sambamba na hilo pia alielezea baadhi ya changamoto wanazo kabiliana nazo kuwa ni kushindwa kuyafikia maeneo yote yanayoendeshwa michuano hiyo kutokana na jografia ya wilaya hiyo na miundombinu isiyo rafiki.

"Tumekuwa tukiwasiliana na wenzetu wanaoongoza mashindano katika kila kata lakini changamoto kubwa inakuja ni jinsi ya kuyafikia maeneo kwani kunatokea changamoto kutokana na jografia ya wilaya yetu pamoja na miundombinu isiyo rafiki kwa kufika huko inapelekea kutofika kwa wakati hivyo tunalazimika kuahirisha mechi mpaka tutakapotatua changamoto hiyo", Alisema Haule.

Aidha kwa upande wa washiriki wa mashindano hayo wamekiri kufurahishwa na michuano hiyo ambapo ni michuano ambayo inaimarisha ushirikiano baina ya vijana sanjari na kufanya afya zao kuwa bora zaidi.

Nasibu Luoga ni mmoja wa washiriki hao amesema kuwa wana kila sababu ya kuwaletea mashindano hayo kwani ni makubwa na yanayotumia gharama nyingi sana.

Amesema kuwa kuwaomba wadau mbalimbali kujitokeza kwa wingi na kumuunga mkono mbunge huyo kwa kile anachofanya ili kuweza kuimarisha mashindano haya."Tunaomba mjitokeze wadau wengi zaidi ili kuunga mkono juhudi hizi zinazofanywa na mbunge wetu katika kuongeza nguvu zaidi za kuimarisha vijana", Alisema Luoga.

Akizungumzia mashindano hayo mbunge huyo amesema kuwa katika kufanikisha mashindano hayo ametoa jezi seti 140 pamoja na mipira 140 vyenye thamani ya shilingi Milioni 28.
Amesema mashindano hayo yatakapo kamilika Katika ngazi ya kata timu itakayoibuka mshindi itajinyakulia kitita cha shilingi laki moja pamoja na kombe litakaloandikwa jina la kata huku mshindi wa pili akijinyakulia shilingi elfu hamsini.

"Mashindano haya ni endelevu ambapo yatakuwa yakifanyika kila mwaka na watakuwa wakishindania vikombe hivi ambavyo vinatolewa katika kila kata huku katika ngazi ya tarafa na wilaya zikishindaniwa zawadi nyingine zaidi". Alisema Kamonga.

Ameongeza kuwa timu zitakazoshinda kwa ngazi ya tarafa na wilaya zitapewa zawadi kubwa zaidi kuliko zilizotolewa kwa washindi wa ngazi ya kata.

Baadi ya wachezaji wa ligi ya mbunge wakiwa katikakati ya uwanja wa mpira wa wilaya ya Ludewa.
Michuano ya ligi ya mbunge wilayni Ludewa mkoani Njombe ikiendelea katika kata mbalimbali
Baadhi ya wachezaji wa ligi ya mbunge wakiwaapunziko ligi kuanza tena


 

1 comment:

  1. Awesome and interesting article. Great things you've always shared with us. Thanks. Just continue composing this type of post.

    ReplyDelete

Post Bottom Ad