HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 31, 2021

VIJIJI 85 SINGIDA VYANUFAIKA NA MRADI WA BORESHA LISHE

 

Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, wakiwa na kabrasha lenye maelezo ya Mradi wa Boresha Lishe baada ya kukabidhiwa rasmi mradi huo  katika Kijiji cha Sekeutoure Wilayani Singida jana. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri  hiyo, Eliya Digha, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Hassan  Ngoma, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Rashid Mandoa, Mwakilishi wa Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Idara ya Afya Kitengo cha Lishe, Mariam Nakuwa, Mwenyekiti wa kijiji hicho Joshua Majengo na Afisa Lishe wa Wilaya hiyo, Neema Swai.


Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Hassan  Ngoma,akihutubia kwenye hafla hiyo.

Afisa Lishe kutoka WFP, Neema Shosho akizungumza kwenye hafla hiyo.
Wawezeshaji wakiwa na bidhaa zao walizozitengeneza kutokana na vyakula vya mbalimbali pamoja na nafaka.

Wananchi wa Kijiji cha Sekeutoure wakiwa kwenye hafla hiyo.

Wananchi wa Kijiji cha Sekeutoure wakiwa kwenye hafla hiyo.
Wananchi wa Kijiji cha Sekeutoure wakiwa kwenye hafla hiyo.
        Mgeni rasmi Katibu wa Wilaya ya Singida, Hassan Ngoma,akiserebuka pamoja na wakina mama.
Mgeni rasmi Katibu wa Wilaya ya Singida, Hassan Ngoma akipata maelezo ya elimu ya utunzaji wa mazingira alipokuwa akitembelea mabanda wakati wa hafla hiyo.
Mgeni rasmi Katibu wa Wilaya ya Singida, Hassan Ngoma (hayupo pichani) akipata maelezo kwenye banda la ufugaji wa wanyama wadogo.
Mgeni rasmi Katibu wa Wilaya ya Singida, Hassan Ngoma  akipata maelezo ya jinsi ya kukausha mbogamboga kwa kutumia kaushio maalumu bila ya kuondoa viini lishe.
Mgeni rasmi Katibu wa Wilaya ya Singida, Hassan Ngoma  akipata maelezo ya jinsi ya kutengeneza  vyakula vya aina mbalimbali. Kulia ni Meneja Mkuu wa Shirika la SEMA, Ivo Manyaku

.Mgeni rasmi Katibu wa Wilaya ya Singida, Hassan Ngoma  akipata maelezo ya jinsi ya kutengeneza  Juisi kwa kutumia nafaka.
Mgeni rasmi Katibu wa Wilaya ya Singida, Hassan Ngoma  akipata maelezo ya jinsi ya kutengeneza  Juisi kwa kutumia nafaka na matunda ya asili.
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Sekeutoure, akizungumza kwenye hafla hiyo.
Afisa Lishe wa Wilaya hiyo, Neema Swai., akizungumza kwenye hafla hiyo.
. Mwenyekiti wa Kijiji cha Sekeutoure., Joshua Majengo.akizungumza kwenye hafla hiyo.
Burudani zikiendelea.
Viongozi wakiwa meza kuu.

 Mwenyekiti wa Halmashauri  hiyo, Eliya Digha, (kushoto)  na Meneja wa Shirika la SEMA, Ivo Manyaku (kulia) wakiserebuka  kwenye hafla hiyo. 


Kwaya ya Boresha Lishe ya Wakina Mama wa Kijiji cha Sekeutoure ikitoa burudani kwenye hafla hiyo.


Mwakilishi wa Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Idara ya Afya Kitengo cha Lishe, Mariam Nakuwa,  akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Rashid Mandoa, akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri  hiyo, Eliya Digha, akizungumza kwenye hafla hiyo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Wananchi wa Kijiji cha Seketoure wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi huku wakionesha furaha yao baada ya kukabidhiwa mradi huo.
 


Na Dotto Mwaibale, Singida

JUMLA ya Vijiji 85 katika Wilaya za Ikungi na Singida  vimenufaika na Mradi wa Boresha Lishe ambao umefadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya (EU) Serikali ya Watu wa Japani na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP)

Mradi huo wa miaka mitano ambao umefikia tamati jana mkoani Singida ulitekelezwa na Serikali ya Tanzania pamoja na wadau watatu Shirika la Sustainable Environment Management Action (SEMA) Research Community and Organizational Development associate (RECODA) na Tanzania Partnership in Nutrition (PANITA) katika mikoa ya Dodoma na Singida.

Akizungumza katika hafla ya kufunga mradi huo iliyofanyika jana Kijiji cha Sekeutoure Wilayani Singida mkoani hapa, Afisa Lishe kutoka WFP, Neema Shosho alisema mradi huo ulijikita katika maeneo matatu makubwa.

Alitaja eneo la kwanza kuwa ni kwenye vituo vya afya  ambavyo walikuwa wakivisaidia kwa kutoa unga wa lishe ambao ulitumika kwa ajili ya kuondoa udumavu pamoja na kutibu udumavu kwa watoto walio chini ya miaka miwili.

"Pia tulikuwa tukitoa elimu ya lishe katika vituo hivyo vya afya, upimaji na ushauri wa masuala ya lishe." alisema Shosho.

Shosho alisema kuwa mradi huo haujaishia kwenye vituo hivyo vya afya pekee pia upo kwenye ngazi ya jamii ambapo kwenye mikoa hiyo miwili kuna vijiji 124 ambavyo vimefikiwa na shughuli mbalimbali za lishe moja ya shughuli hizo ni elimu ya masuala ya lishe bora.

Alisema jamii imefundishwa juu ya vyakula mchanganyiko, unyonyeshaji kwa watoto na umuhimu wa siku 1000 kuanzia mimba inapotunga hadi mtoto atakapokuwa na miaka miwili.

Aidha Shosho alisema kuwa jamii pia imefundishwa namna ya uzalishaji wa chakula mchanganyiko ambapo mradi huo umewapatia mbegu na kulima vyakula hivyo.

Alisema mbali ya kuwapa mafunzo hayo pia walifundishwa namna ya kufuga wanyama wadogo kama sungura na ufugaji wa kuku.

Alisema jamii pia ilifundishwa namna ya kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha vikundi vya kuweka na kukopa (VICOBA) ambavyo vinawasaidia kuhifadhi fedha zao  na kuongeza chakula chenye lishe kwenye kaya.

Alitaja suala lingine kuwa ni la usafi ambalo ni muhimu sana kwani mtu hawezi akawa na lishe bora bila ya kuwepo na usafi ambapo walifundishwa namna ya kutumia vyoo, unawaji wa mikono na teknolojia nyepesi ya kuwezesha kila kaya kuwa na kinawia mikono 'kibuyu chirizi' ambavyo vipo katika kaya iliyofikiwa na mradi huo.

Alisema pia wamewafusha jinsi ya kupika vyakula mchanganyiko na vya lishe bora kutoka kwenye vyakula asili vilivyopo katika maeneo yao yakiwemo matunda na mboga.

Shosho alitaja suala la mwisho kuwa ni la kuzijengea uwezo halmashauri ili ziweze kusimamia mradi huo baada ya kukabidhiwa kwa kusaidia katika vikao vyao kufuatilia shughuli hizo  ukizingatia miradi hiyo ni yao na ipo chini ya Serikali.

"Tunaomba mradi huu muutunze na kama itawezekana ziundwe sheria ndogo ndogo zitakazosaidia kuutunza ili uendelee kuwanufaisha wana Singida hususani katika halmashauri hizo." alisema Shosho.

Mwakilishi wa Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Idara ya Afya Kitengo cha Lishe, Mariam Nakuwa aliyashukuru mashirika yote na halmashauri zilizopitiwa na mradi huo na akaahidi juhudi zote ambazo zimewekezwa kwa  miaka mitano hazitapotea bure na kuwa Serikali itaendelea kuratibu na kusimamia masuala yote ya  lishe.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Rashid Mandoa ameahidi kuyaendeleza mambo yote yaliyofanywa na mashirika hayo kupitia mradi wa Boresha Lishe ambao waliwapa mawazo na wao wamekuwa wanufaika.

Mwenyekiti wa Halmashauri  hiyo, Eliya Digha aliwahimiza wananchi wa Kijiji hicho kulima mahindi yenye rangi ya njano ambayo yanapatika kwenye kijiji hicho cha Seketoure na kuwa yana lishe na bei yake ni kubwa.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho Joshua Majengo alisema baada ya kupata mafunzo hayo kupitia mradi huo udumavu na utapiamlo kwa watoto umepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na awali.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad