HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 25, 2021

MKUU WA MAJESHI APONGEZWA UJENZI WA UWANJA GOFU DODOMA

 Mkuu wa majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara (katikati ) akiwa na baadhi ya wachezaji na wachezaji wasaidizi kwenye Kibanda cha Kupumzikia wachezaji wakati wa zoezi kuzindua kibanda hicho katika Uwanja wa Gofu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo Jijini Dar es Salaam jana.

Mkuu wa majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara (Katikati) akizindua jiwe la msingi kwenye Uwanja wa gofu wa jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania ya Lugalo Dar es Salaam wanaomtazama ni Mwenyekiti wa Lugalo Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo wa kwanza kulia , balozi Ombeni Sefue, Profesa Wineaster Anderson na wakwaza kushoto ni Dk Edmund Mdolwa.
Mkuu wa majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara (wapili kulia) akikata Utepe kwenye Kibanda cha Kupumzikia wachezaji kulia kwake ni Mwenyekiti wa Klabu ya Golf Lugalo Brigedia jenerali Mstaafu Michael Luwongo ,Balozi Ombeni Sefue, Nahodha wa Lugalo Kapteni Japhet Masai na Wakwanza kulia ni Joseph Kitani Mchezaji wakati wa zoezi katika uwanja wa jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania ya Lugalio Jijini Dar es Salaam jana.

Na.Kapteni Selemani Semunyu JWTZ
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo amepongwezwa kwa Jitihada za Kujenga Uwanja wa Golf Jijini Dodoma.

Hayo yalisemwa Jana na Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara wakati akizindua kivuko na kibanda cha kupumzikia Wachezaji wakati wa Mazoezi katika Uwanja wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.

" Mwanzo tulipata eneo yatakapojengwa Malao Makuu ya Jeshi Dodoma lakni ilikuwa mbali lakini kwa Kilimani ni eneo sahihi, " Alisema General Waitara.

Jenerali Mstaafu Waitara aliongeza kuwa uwanja huo kujengwa itamfanya Mkuu huyo wa Majeshi kuacha kumbukumbu kubwa kati ya kumbukumbu za Heshima alizoziacha.

"Jeshi ni mfano na linaongoza katika kuhamasisha Michezo yote nchini na halijawahi kushindwa hivyo ni mwendelezo huo ni mzuri. alisema Jenerali Mstaafu Waitara.

Aliongeza kuwa Ujenzi wake sio mgumu na kinachotakiwa kufanyika ni kuchukua kilichofanyika klabu ya golf ya Lugalo kuhamishia Dodoma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Klabu ya Lugalo Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo alipongeza Wanachama wanaojitoa kutatua changamoto za Uwanja.

Aidha alitoa Wito kwa Wachezaji wengine wwnye nia njema kujitokeza kusaidiana kutatua Changamoto mbalimbali zinazojitokeza Uwanjani.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Timu ya Majenerali na Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dk Edmund Mndolwa amewaomba viongozi wa Selikali kucheza Mchezo huo.

Alisema Golf ndio Mchezo Pekee unaoweza kucheza kwa Muda Mrefu bila kujali Umri na idadi.

Ujenzi wa Kidaraja umefanikishwa kwa hisani ya proffesa Wineaster .......na Kibanda cha Pumzikia ni Mike Laizer.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad