HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 21, 2021

MAKATIBU WAKUU OFISI YA MAKAMU WA RAIS WAFANYA ZIARA ZANZIBAR

 

 
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Ngelela Maganga (katikati) akizungumza na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Bi. Khadija Khamis Rajab alipotembelea Ofisi hiyo akiwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Mohammed Khamis Abdulla (kushoto).
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Ngelela Maganga akiwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi hiyo Bw. Mohammed Khamis Abdulla wakiagana na viongozi wa Tume ya Pamoja ya Fedha (JFC) walipotembelea Ofisi hiyo Zanzibar.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga (wa pili kulia) akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili (Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi) Dkt. Khalid Salum Mohamed alipokutana naye katika ukumbi wa wageni uliopo katika Ofisi za Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Wengine pichani kuanzia kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Mohammed Khamis Abdulla, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Bw. Thabit Idarus Faina na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Tixon Nzunda.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Ngelela Maganga akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo katika Ofisi ya Zanzibar alipofanya ziara akiwa na Naibu Katibu Mkuu Bw. Mohammed Khamis Abdulla.
Kuanzia kushoto Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Ngelela Maganga akiwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi hiyo Bw. Mohammed Khamis Abdulla, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais (Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi) Zanzibar Bw. Thabit Idarus Faina na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Tixon Nzunda wakibadilishana mawazo katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi wakati wa ziara yao.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Ngelela Maganga akiwa na viongozi wengine na wadau wa mazingira kutoka sekta binafsi walipotembelea mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi eneo la Kilimani Mkoa wa Mjini Magharibi.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad