HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 12, 2021

BARABARA YA HAYDOM-MBULU KUJENGWA KWA LAMI

 

 Na Mwandishi wetu, Mbulu

NAIBU Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Godfrey Kasekenya amewaahidi wananchi wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, kuanzwa kwa ujenzi wa kilomita 50 za barabara ya lami ya Haydom-Mbulu.

Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 389 imeanzia wilayani Karatu mkoani Arusha, Mbulu- Haydom mkoani Manyara, Sibiti-Lalago mkoani Simiyu, hadi Kolandoto mkoani Shinyanga.

Naibu Waziri Kasekenya amesema barabara hiyo ya lami itaanza kujengwa kilomita 50 kwenye mwaka huu wa fedha unaoishia mwezi Juni mwaka huu.

 Amesema wataanza kujenga barabara hiyo ili kutimiza ahadi ya Rais na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa CCM ambayo imetamka ujenzi wa barabara hiyo.

 "Ahadi zilizotolewa na hayati John Magufuli zitaendelea kutekelezwa na Serikali inayoongozwa na Rais wetu Samia Suluhu Hassan hivyo barabara hii nayo itajengwa kama ilivyoahidiwa kwenu," amesema Kasekenya.

 Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Dokta Chelestino Simbalimile Mofuga amemshukuru Naibu Waziri Kasekenya kulia kwa kuwapa ahadi hiyo kwani wananchi wataondokana na kero ya barabara.

 Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Fratei Maasay amesema barabara hiyo inatumika kusafirisha mazao, abiria na wengine kupelekwa hospitali ya rufaa ya Haydom kupata matibabu.

 Mbunge wa Jimbo la Mbulu mjini, Paul Isaay ameishukuru Serikali kwa kujenga daraja la mto Magara linalounganisha wilaya za Mbulu na Babati, hivyo ujenzi wa barabara ya lami ya Mbulu-Haydom itachochea maendeleo.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Godfrey Kasekenya akizungumza na wananchi wa Kata ya Magara alipotembelea na kukagua daraja la Magara linalounganisha Wilaya za Babati na Mbulu Mkoani Manyara.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Godfrey Kasekenya akizungumza na wananchi wa Kata ya Haydom Mkoani Manyara juu ya ujenzi wa barabara ya lami, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Dokta Chelestino Simbalimile Mofuga na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Flatei Maasay.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Godfrey Kasekenya (kulia) akikagua daraja la Magara linalounganisha Wilaya za Babati na Mbulu Mkoani Manyara.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad