HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 17, 2021

MAWASILIANO KUPELEKWA BANDARI YA KALEMA - NAIBU WAZIRI KUNDO

 


Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea akizungumza katika Bandari ya Kalema alipokwenda kuangalia fursa za kupeleka mawasiliano katika Bandari hiyo iliopo Ziwa Tanganyika wilayani Tanganyika mkoani Katavi.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea akimsikiliza Mkandarasi Mshauri katikq Bandari ya Kalema iliyopo Ziwa Tanganyika mkoani Katavi alipokwenda katika ziara kuangalia hali ya mawasiliano.
Naibu Waziri  wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea akiwa na Kamati ya Ulizi na Usalama Mkoa wa Katavi  kwenye ujenzi wa Bandari ya Kalema katika Ziwa Tanganyika wilayani Tanganyika ikiwa ni ziara ya kuangalia fursa za mawasiliano katika Bandari hiyo.
Hapa Ziwa Tanganyika katika Mkoa wa Katavi inayojengwa Bandari ya Kalema kwa usafirishaji kutoka Tanzania kwenda Nchini Congo.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Katavi.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  Jamila Yusuph akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi kuhusiana ziara ya Naibu Waziri na Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea katika Mkoa wa  Katavi.
Naibu Waziri Kundo akiangalia ujenzi wa Bandari ya Kalema.
Naibu Waziri  Kundo akiangalia ramani ya Ujenzi wa Bandari ya Kalema.
 

*Ni Mawasiliano ya Mkongo wa Taifa  pamoja mawasiliano ya simu kuanzia 3G 

Na Chalila Kibuda, Michuzi Tv - Tanganyika 

NAIBU Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrea amesema kuwa bandari ya Kalema inayojengwa  Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi pindi inapokamilika inahitaji kuwa mawasiliano ya mkongo wa Taifa kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano hapo.

Kundo ameyasema hayo wakati wa ziara ya kuangalia hali ya Mawasiliano katika Mkoa wa Katavi kwa kufika katika Bandari ya Kalema kuona fursa za kuweka mawasiliano kutokana huduma nyingi zitakuwa za mtandao.

Amesema kuwa  Serikali imefanya kazi kubwa ikiwemo ujenzi wa bandari kwa kodi za wananchi hivyo kila sehemu inahitaji kuwa na mawasiliano yenye ubora.

Naibu Waziri  Kundo amesema kuwa sehemu zote ambazo zinahitaji kufanyiwa maboresho zifanyiwe kazi sio za kuandika bila utekelezaji.

"Tunahitaji kufanya kazi kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kuweza kupata maendeleo katika kutimiza ndoto ya Rais Daktari John Pombe Magufuli ya kuanzisha Wizara mpya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari"amesema Mhandisi Kundo.

Aidha amesema kabla ya serikali kwa upande wa Ziwa Tanganyika na Wilaya ya Tanganyika ilikuwa haina mvuto wa kibiashara lakini sasa kumegeuka fursa kwa kampuni za mawasiliano kuwekeza pamoja na minara iliyojengwa kuongeza uwezo wa 3G ili kuweza kutumia data.

Mhandisi Kundo amesema kuwa Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo zinatakiwa kufanya kazi pamoja na kuwa wabunifu wa kutatua changamoto za wananchi na wale wanaofanya biashara wafanye kiushindani kwa kuzalisha.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi ,Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amesema kuwa ziara ya Naibu Waziri imejibu changamoto za mawasiliano pamoja na elimu ya kazi ya Wizara hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad