Mwenyekiti
wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Ngassa Mboje akifungua
Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya
Shinyanga kwa Robo ya Pili ya mwaka 2020/2021
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Ngassa Mboje amewataka
madiwani kuhamasisha wananchi kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa na
madawati ili kumaliza changamoto ya wanafunzi kukaa chini.
Mboje
ameyasema hayo leo Jumanne Februari 16,2021 kwenye Mkutano wa Kawaida
wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa Robo ya
Pili ya mwaka 2020/2021 uliofanyika katika Makao Makuu ya Halmashauri ya
Wilaya ya Shinyanga Iselamagazi – Nindo ukiwa na lengo la kujadili
miradi inayotekelezwa katika halmashauri hiyo.
Mwenyekiti
huyo wa Halmashauri alisema ili kumaliza changamoto ya vyumba vya
madarasa na madawati, Madiwani wanayo nafasi kubwa ya kuwahamasisha
wananchi kuchangia badala ya kusubiri serikali ifanye kila kitu.
“Halmashauri
ya wilaya ya Shinyanga tunataka kutoka kwenye hali ya wanafunzi kukaa
chini. Hamasisheni wananchi kuchangia madawati. Lakini pia hakikisheni
viongozi wa vitongoji wanashirikishwa katika mambo ya maendeleo ikiwa ni
pamoja na kuwapa taarifa kuhusu fedha za zinazotoka serikali kuu kwa
ajili ya miradi ya maendeleo”,alisema Mboje.
Katika
hatua nyingine aliwataka TANESCO, RUWASA, TARURA na Idara ardhi wawe na
mawasiliano kwa sababu wote wanafanya kazi ya jamii katika kuweka
vizuri miundo mbinu.
Naye
Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Christina Mnzava alisema ili kupiga hatua
za kimaendeleo ni lazima madiwani na wabunge na watendaji wa serikali
washirikiane.
Aidh
aliwasihi madiwani wa halmashauri hiyo kujiunga na Mifuko wa Bima ya
Afya na kuomba Mfuko wa bima ya afya kutoa mkopo wa vifaa tiba kwenye
hospitali na vituo vya afya.
Katika
Mkutano huo, madiwani wamepaza sauti kuhusu changamoto ya ubovu wa
miundombinu ya barabara ambapo baadhi ya barabara zimekatika na madaraja
hayapitiki hivyo kuiomba Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA)
kuzifanyia kazi barabara zinazolalamikiwa.
Walizitaja
baadhi ya barabara zinazotakiwa kufanyiwa kazi kuwa ni pamoja na
Barabara ya kutoka Didia – Solwa, Imenya – Usule- Mwamala na madaraja ya
Nduguti – Igembya na Mimbi – Ikota na maeneo mengine ikiwemo
miundombinu ya barabara katika Mji wa Didia.
Suala
jingine lililoibuka katika mkutano huo ni changamoto ya miradi ya maji
kutokamilika kwa wakati na miradi kutoendana na mikataba.
Diwani
wa kata ya Mwakitolyo, Masalu Nyese aliiomba RUWASA kuongeza kasi ya
utekelezaji wa mradi wa maji katika kata hiyo ambao umekuwa ukisuasua na
hivi sasa umesimama kwa takribani wiki mbili kutokana na upungufu wa
mabomba hali inayosababisha wananchi kuendelea kukabiliwa na changamoto
ya maji.
Masalu
ametumia fursa hiyo kumuomba Mwekezaji katika mgodi wa Mahiga kuajiri
vijana kwa mkataba maalumu badala ya utaratibu uliopo sasa ambao
haueleweki.
Akizungumza
katika mkutano huo, Meneja wa TARURA wilaya ya Shinyanga Mhandisi
Salvatory Yambi alisema watatembelea barabara zenye changamoto na
kuchukua hatua huku Kaimu Meneja Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) wilaya
ya Shinyanga Emmael Nkopi akisema wataendelea kutekeleza miradi ya
maji kama inavyotakiwa.
ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambaye ni Diwani wa kata ya
Mwalukwa Mhe. Ngassa Mboje akifungua Mkutano wa Kawaida wa Baraza la
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa Robo ya Pili ya mwaka
2020/2021 uliofanyika katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya
Shinyanga Iselamagazi – Nindo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa
Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambaye ni Diwani wa Kata ya
Iselamagazi Mhe. Isack Sengelema. Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya
wilaya ya Shinyanga Mhe. Hoja Mahiba. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambaye ni Diwani wa kata ya
Mwalukwa Mhe. Ngassa Mboje akifungua Mkutano wa Kawaida wa Baraza la
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa Robo ya Pili ya mwaka
2020/2021
Makamu
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambaye ni Diwani wa
Kata ya Iselamagazi Mhe. Isack Sengelema akizungumza kwenye Mkutano wa
Kawaida wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa
Robo ya Pili ya mwaka 2020/2021 uliofanyika katika Makao Makuu ya
Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Iselamagazi – Nindo.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Mhe. Hoja Mahiba akizungumza
kwenye Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya
ya Shinyanga kwa Robo ya Pili ya mwaka 2020/2021
Mbunge
wa Viti Maalumu Mhe. Christina Mnzava akizungumza kwenye Mkutano wa
Kawaida wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa
Robo ya Pili ya mwaka 2020/2021
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Ngassa Mboje akiongoza
Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya
Shinyanga kwa Robo ya Pili ya mwaka 2020/2021
Afisa Uanachama NHIF mkoa wa Shinyanga, Errison Halinga akiwaelezea Madiwani kuhusu umuhimu wa bima ya afya
Meneja wa TARURA wilaya ya Shinyanga Mhandisi Salvatory Yambi akielezea kuhusu miradi ya barabara
Kaimu Meneja Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) wilaya ya Shinyanga Emmael Nkopi akielezea kuhusu miradi ya maji
Madiwani wakiwa ukumbini
Madiwani wakiwa kwenye kikao
Diwani wa kata ya Mwakitolyo, Masalu Nyese akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani.
Diwani wa kata ya Solwa, Awadhi Mbaraka akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
No comments:
Post a Comment