HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, January 8, 2021

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA CHINA WANG YI ATEMBELEA MWALO WA SAMAKI WA CHATO,AFANYA MAZUNGUMZO RASMI NA TANZANIA

 

 


 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Mashimba Ndaki akimpatia maelezo Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi kuhusu samaki wa aina mbalimbali na minofu yao wanaopatikana katika Ziwa Victoria wakati mgeni huyo alipotembelea Mwalo wa Chato mkoani Geita mapema asubuhi ya leo Ijumaa Januari 8, 2021.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Mashimba Ndaki na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi wakipata maelezo kuhusu minofu ya samaki wanaopatikana katika Ziwa Victoria wakati mgeni huyo alipotembelea Mwalo wa Chato mkoani Geita mapema asubuhi ya leo Ijumaa Januari 8, 2021
Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi akiongea na wavuvi na wadau wengine wa sekta ya uvuvi alipotembelea na mkujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika katika Mwalo wa samaki la Chato Mkoani Geita alikotembelea leo Ijumaa Januari 8, 2021 ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake nchini
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi akimkaribisha rasmi nchini Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi na ujumbe wake kabla ya kufanyika mazungumzo rasmi wa pande hizo mbili mjini Chato mkoa wa Geita leo Ijumaa Januari 8, 2021 ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake nchini

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad