HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 28, 2021

TAASISI YA FLAVIAN MATATA YATOA UFADHILI WA TAULO ZA KIKE KWA WASICHANA 1000 KWA MWAKA MZIMA

 

Mgeni rasmi Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Abdul Maulid pamoja na  Mwanamitindo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Flaviana Matata, Flaviana Matata  akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi, walimu, maafisa elimu wa wilaya zote za Dar es Salaam pamoja na wadau mbalimbali wa masuala ya mtoto wa kike mara baada ya kufanyika kwa uzinduzi wa ufadhili wa elimu kwa wasichana 1000 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na kati yao wasichana 250 wanatoka Mkoa wa Dar es Salaam ambao pia watapata  taulo za kike za Lavy bure kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kuanzia. 

Katika jitihada za kuendelea kuisaidia jamii hasa mtoto wa kike Mwanamitindo na Mjasiriamali Flaviana Matata chini ya taasisi yake ya ‘Flaviana Matata Foundation’ ambayo ilianzishwa kwa lengo la kusomesha watoto wa kike watokao kwenye mazingira magumu pamoja na kuhamasisha upatikanaji wa elimu bora katika mazingira rafiki na salama kwa wanafunzi kupitia utoaji wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia, ujenzi na ukarabati wa vyoo, madarasa, ofisi na nyumba za walimu.

Leo Flaviana amezindua rasmi ufadhili wa elimu kwa wasichana 1000 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na kati yao wasichana 250 wanatoka Mkoa wa Dar es Salaam ambao pia watapata  taulo za kike za Lavy bure kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kuanzia. Msaada huu umelenga kuhakikisha hedhi kutokua kikwazo kwa watoto wa kike wa Kitanzania kupata elimu bora itakayoweza kuwajengea misingi imara ili waweze kuzifikia ndoto zao kupitia.

Ufadhili huu umepatikana baada ya kuchangisha pesa kupitia kampeni ya ‘Donate A Period’ iliyofanywa na Flaviana pamoja na baadhi ya marafiki zake nchini Marekani kwa lengo la kuhakikisha watoto wa kike hawakosi masomo kwasababu ya kutomudu gharama za taulo za kike(Sanitary Pads).

Akiongea na wana habari Flaviana amesema “Kuna watoto wengi hasa wakike ambao wapo kwenye mazingira magumu na wanakosa haki yao ya msingi ya kupata elimu bora kutokana na changamoto walizonazo. Hivyo nafurahi sana tumeweza kufanikisha ufadhili huu  kwa mabinti 1000 ambao kwa namna moja au nyingine ufadhili huu utaenda kubadilisha maisha yao hasa wakiwa shuleni”

Flaviana ameongeza pia “Natamani ufadhili huu uwe ni mwanzo tu wa kuhamasisha na kushawishi serikali, makampuni binafsi na jamii kwa ujumla kuunga mkono juhudi hizi ili kupitia Flaviana Matata Foundation tuweze kuwafikia na kuwasaidia watu wengi zaidi wenye uhitaji ambayo hii itasaidia pia kuinua jamii zetu na nchi yetu kwa ujumla” 

“Inapendeza sana kuona juhudi mbalimbali zinazofanywa na watu binafsi katika kuboresha maisha ya watanzania hasa kwenye upande wa Elimu na kwa watoto wakike. Itapendeza sana kama watu mbalimbali wakijitokeza kusaidia juhudi hizi zifike mbele zaidi kwa chochote kile au vyovyote vile tujaribu kushiriki kwenye  kuwainua mabinti lakini kuinua nchi yetu ambayo inahitaji kila mtu kuwajibika ili iende mbele” aliongea mgeni rasmi Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Abdul Maulid aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abubakar Kunenge. 

Kipekee kabisa Flaviana Matata anawashukuru marafiki zake waliochangia kwenye kampeni hii ya ‘Donate A Period’ kwa kufanikisha hili, Mkuu wa mkoa kwa kukubali kuwa mgeni rasmi, wakuu wa wilaya , wakurugenzi, maafisa elimu na watu wote waliofanikisha shughuli hii. 


Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Abdul Maulid akizungumza na wanafunzi, walimu na maafisa elimu wa wilaya zote za Dar es Salaam wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa ufadhili wa elimu kwa wasichana 1000 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na kati yao wasichana 250 wanatoka Mkoa wa Dar es Salaam ambao pia watapata  taulo za kike za Lavy bure kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kuanzia. Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Abdul Maulid alimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Abubakar Kunenge.
Mwanamitindo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Flaviana Matata, Flaviana Matata akizungumza na wanafunzi, walimu na maafisa elimu wa wilaya zote za Dar es Salaam wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa ufadhili wa elimu kwa wasichana 1000 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na kati yao wasichana 250 wanatoka Mkoa wa Dar es Salaam ambao pia watapata  taulo za kike za Lavy bure kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kuanzia. 
Baadhi ya wanafunzi, walimu, maafisa elimu wa wilaya zote za Dar es Salaam pamoja na wadau mbalimbali wa masuala ya mtoto wa kike wakifuatilia hotuba ya Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Abdul Maulid alimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Abubakar Kunenge wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa ufadhili wa elimu kwa wasichana 1000 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na kati yao wasichana 250 wanatoka Mkoa wa Dar es Salaam ambao pia watapata  taulo za kike za Lavy bure kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kuanzia. 
Mwanamitindo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Flaviana Matata, Flaviana Matata akikabidhi taulo za kike za Lavy kwa Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Abdul Maulid zitakazokuwa zinatolewa kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mzima katika shule zilizopo jijini Dar es Salaam.
Mwanamitindo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Flaviana Matata, Flaviana Matata akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali zilizopo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa ufadhili wa elimu kwa wasichana 1000 kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na kati yao wasichana 250 wanatoka Mkoa wa Dar es Salaam ambao pia watapata  taulo za kike za Lavy bure kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kuanzia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad