Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imesema kuwa itatumia pambano la bondia
Ibrahim Class na Dennis Mwale wa Zambia (Rhumbo in Dar) kuutangaza
utalii wa nchi nje ya mipaka yake.
Bondia wa Tanzania, Class na
Mwale watapambana Ijumaa kwenye ukumbi wa Next Door Arena wa Masaki
kuwania ubingwa wa mabara wa WBF wa uzito wa Super Feather.
Pambano
hilo limeandaliwa na kampuni ya Jackson Group Sports na litaoneshwa
nchi zaidi ya 150 duniani. Siku hiyo pia kutakuwa na mapambano mengine
nane yalishirikisha mabondia mbalimbali ikiwa pamoja na bondia nyota wa
Bulgaria, Tervel Pulev ambaye amewasili pamoja na bondia nyota wa uzito
wa juu duniani Kubrat Pulev ambaye alipigana na Anthony Joshua mwishoni
mwa kwaka jana.
Mkurugenzi wa Masoko wa TTB, Mindi Kasiga amesema
jana kuwa watatumia fursa hiyo kuutangaza utalii wa nchi kwani
mapambano ya ngumi hayo yataonekana nchi nyingi.
“Hii ni fursa kwetu kuutangaza utalii na kuingia kusapoti Jackson Group Sports,” alisema Kasiga.
Mbali
ya TTB, pambano hilo limedhaminiwa na benki ya CRDB ambapo meneja wa
chapa, Joe Bendera alisema kuwa wanazidi kuendeleza michezo nchini kwani
walidhamini pia mpira wa kikapu, kuandaa marathoni na kutoa fursa ya
masomo kwa vijana 26 kupitia mpira wa kikapu.
Kwa upande wake,
Afisa Mtendaji Mkuu wa Global Boxing Stars (GBS), Scott Farrell alisema
kuwa wamevutiwa na kampuni ya Jackson Group Sports na kuamua kufanya nao
kazi pamoja kuinua mhezo wa ngumi za kulipwa.
Alisema kuwa lengo
lao ni kuinua vipaji vya mchezo huo hapa nchini. Mbali ya wadhamini
hao, wadhamini wengine ni Azam TV, Onomo Hotel, Precision Air, Vitasa,
Bono 5, Hotel Demag na Henessy.
Mkurugenzi Mtendaji a Jackson
Group Sports, Kelvin Twissa alisema kuwa maandalizi ya pambano hilo
yamekamilika na mabondia wote wamewasili kwa ajili ya kuzichapa Ijumaa.
Twissa alisema kuwa kila bondia ana ari kubwa ya kushinda katika pambano hilo.
Mkurugenzi
wa kampuni ya Jackson Group Sports, Kelvin Twissa (wa pili kulia)
akizungumza wakati wa mkutano wa maandalizi ya mwisho ya pambano baina
ya bondia Ibrahim Class na Dennis Mwale wa Malawi kuwania ubingwa wa
mabara wa WBF. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa bodi ya Utalii, Mindi
Kasiga na wengini ni Meneja Chapa wa benki ya CRDB, Joe Bendera (wa
kwanza) kushoto na Afisa Mteandji Mkuu wa GBS, Scott Farrell
Bondia kutoka Bulgaria Tervel Pulev akiwasili nchini tayari kwa pambano la Ijumaa kwenye ukumbi wa Next Door Arena.
Bondia
kutoka Bulgaria Tervel Pulev (kushoto)akiwa na kaka yake, Kubrat Pulev
wakiwasili nchini tayari kwa pambano la Ijumaa kwenye ukumbi wa Next
Door Arena. Kubrat alipambana na Anthony Joshua mwaka jana mwishoni.
Bondia kutoka marekani, Shawn Miller (wa kwanza kulia) akiwasili
tayari kwa pambano la Ijumaa kwenye ukumbi wa Next Door Arena, Masaki.
Tuesday, January 26, 2021
Pambano la Class-Mwale lapamba moto, mabondia watua Dar
Tags
# HABARI MICHEZO
HABARI MICHEZO
Labels:
HABARI MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment