MAKANDARASI
nchini wametakiwa kuwa wanasoma mikataba yao kwa makini kabla ya
kuisaini ili waweze kutambua wajibu wao wakati wa utekelezaji wa mkataba
husika.
Pia wameaswa kuwa wanaurudia mkataba wao mara kwa mara
pindi wakiwa wanaufanya kazi ili kujua kama bado kwenye njia sahihi ama
wa wanatoka nje ya mkataba.
Msajilil wa Bodi ya Wakandarasi,
Rhoben Nkori ameyasema hayo leo Januari 29, 2021 wakati akifunga mafunzo
ya siku tatu kwa makandarasi kujifunza namna ya kusimamia mikataba,
bima na matumizi ya mtandao (Taneps) yaliyoandaliwa na Bodi ya
Wakandarasi (CRB) nchini
"Mafunzo haya ni muhimu sana kwa
makandarasi kwa sababu suala la usimamizi wa mikataba ni muhimu sana na
ndio unaamua utekelezaji mzima wa mkataba kwani ukishindwa kutumia
mkataba maana yake unashindwa kujua haki zako na wajibu wako katika
kufanya kazi" amesema Nkori.
"Kuna suala la kusaini, pia kuna
suala la kusoma mikataba ukaijua, ukajua wajibu wako ni nini katika
mkataba huo na kujua haki zako ni nini na kama zimeainishwa vizuri
kwenye mkataba na baada ya kuelewa unaingia mkataba ukishasaini
unautekeleza kwa kufuata mkataba" ameongeza.
Kwa upande wake
mkandarasi Idrisa Kinyagu kutoka kampuni ya ukandarasi ya Powers and
Network Backup Ltd ya jijini Dar es Salaam amesema, mafunzo hayo
yamekuwa msaada mkubwa kwao makandarasi
Tumejifunza namna ya kusimamia mikataba yetu, bima na jinsi ya kutumia mfumo wa kuwasilisha zabuni kupitia mtandaoni.
Mifumo
hiyo mitatu ambayo CRB wametufundisha imetupa mafanikio makubwa sana,
kwa sababu kuna sehemu tulikuwa na matatizo ya namna ya kusimamia
mikataba yetu na wateja, Lakini kupitia mafunzo haya, tumepata maarifa
ambayo yatatusaidia kuhakikisha namna ya kufanikisha kazi kwa ufanisi
kati ya mkandarasi yoyote na mteja pindi mnapoingia mkataba.
Vilevile
katika suala la matumizi ya bima na mtandao tumejifunza vingi, saizi
mtu unaweza ukapata zabuni mtandaoni na kumalizana nayo moja kwa moja
bila ya
kulazimika kwenda mwenyewe kuipeleka na kupoteza muda.
Naye,
Philomena Malenda, mkandarasi kutoka kampuni ya wakandarasi ya
Progressive Women ameishukuru CRB kwa kuwapatia mafunzo hayo, na sasa
wanajua nini cha kufanya pindi wakiingia mkataba hata kama wakikutana na
changamoto mbali mbali.
"Kwa kweli, Taneps imetusaidia kwa kiasi
kikubwa sana ukilinganisha na zamani ambapo sasa inatusadia matumizi ya
muda na kuepuka mlolongo mrefu wa kufikisha zabuni yako kwa kuwa
ukitumia mtandao kazi yako inafanyika mahali popote pale, ameongeza
kuwa serikali inawasaidia sana.
Msajili wa Bodi ya Wakandarasi nchiji, Rhoben Nkori akizungumza na makandarasi wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa makandarasi ya kuwapa maarifa namna ya kusimamia mikataba yao, matumizi ya bima na kutumia mitandao kupata Zabuni. yaliyofanyika jjjini Dar es Salaam
Mkandarasi kutoka kampuni ya wakandarasi ya Progressive Women, Philomena Malenda akizungunza na waandishi wa habari kuelezea namna atakavyoyatumia mafunzo waliyopatiwa na CRB katika kufanikisha kazi zao hususani mikataba watakayoingia
Idrisa Kinyagu kutoka kampuni ya wakandarasi ya Power and Network Backup ltd ya jijini Dar es Salaam, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza mafunzo ya siku tatu yaliyoandaliwa na CRB jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment