Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo Kutoka
kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji
Mbinga, Grace Quintine (kushoto) kuhusu
ukumbi wa Halmashauri ya Mji Mbinga wakati alipofungua jengo la Halmashauri
hiyo, Januari 4, 2021. Wa pili kushoto ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa
na wa tatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme. (Picha
na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme wakifungua
Jengo la Ofisi za Halmashauri ya Mji Mbinga, Januari 4, 2021.(Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kukagua nyumba ya makazi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga , Januari 4, 2021. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Mshenye. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Nyumba za Wakuu wa Idara za Halmashauri ya wilaya ya Mbinga ambazo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alizikagua Januari 4,2020.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa Mkoa wa Ruvuma wakati alipokagua nyumba 7 za Wakuu wa Idara za Halmashauri ya Mji wa Mbinga zilizojengwa na Serikali kwa gharama ya sh. Milioni 321.771, Januari 4, 2021. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
No comments:
Post a Comment