HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 11, 2021

Benki ya CRDB yawazadia wateja 20 ada ya jumla shilingi Milioni 30

Meneja Mwandamizi Ukusanyaji wa Amana Benki ya CRDB, Abel Lasway (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza washindi Kampeni ya Benki hiyo iliyotambulika kama "Tumekusoti Ada" iliyoendeshwa katika kipindi cha mwezi wa Disemba kwa wateja waliofungua akaunti ya watoto (Junior Jumbo) na kuweka akiba ambapo jumla ya wateja 20 wameibuka washindi. Wengine pichani ni Meneja Mauzo wa Benki ya CRDB, Elikira Nkya (kulia) pamoja na Meneja Mahusiano wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya CRDB, Bupe Makibi . 

Benki ya CRDB imetangaza washindi wa promosheni ya “Tumekusoti Ada” iliyozinduliwa na Benki hiyo mapema mwezi Disemba ikilenga katika kuhamasisha wazazi/ walezi kujenga utamadani wa kuwawekea akiba watoto wao kupitia Akaunti ya Junior Jumbo (JJ). 

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Meneja Mwandamizi Ukusanyaji wa Amana Benki ya CRDB, Abel Lasway amesema jumla ya shilingi milioni 30 zimetolewa kama zawadi ya ada kwa washindi 20 ambapo kila mmoja amepatiwa shilingi milioni 1.5.

Akielezea namna ambavyo washindi hao wamepatikana Lasway alisema zawadi zimetolewa kwa wazazi ambao wamekuwa wakiweka akiba mara kwa mara katika akaunti ya Junior Jumbo ya watoto wao.

 “.. tumefanya hivi ili kujenga utamaduni wa kwa wazazi/ walezi kuwawekea watoto wao akiba. Hii inasaidia wazazi kumudu gharama zote zinazohusu watoto ikiwamo ada, matibabu na gharama nyinginezo bila shida yoyote,” alisema Lasway.

Lasway alisema wazazi wengi wamekuwa wakipata changamoto katika kulipa ada za watoto kutokana na wengi kutokuwa na utamaduni wa kuweka akiba kwa ajili ya watoto. Hali hiyo imepelekea watoto wengi kuchelewa kurudi shule kuendelea na masomo au kujiunga na shule kwa wanafunzi wapi kutokana na kukosa kwa mahitaji ya msingi ikiwamo ada.

“Tuna akaunti maalum kwa ajili ya kusaidia wateja kuweka akiba kwa ajili ya watoto, na hii si nyengine ni akaunti ya Junior Jumbo, ni akaunti ambayo inafunguliwa kwa vigezo nafuu sana, haina makato yoyote na hutoa faida ya riba kwa mteja,” anasema Adili huku akisisitiza kuwa Benki ya CRDB imejipanga kutoa elimu kwa wazazi ili kuwasaidia kuishi ndoto za watoto wao kwa kumuwezesha kupata elimu bora.

Lasway alitoa rai kwa wazazi ambao bado hawajawafungulia akaunti watoto wao kutembelea matawi ya Benki ya CRDB yaliyopo nchi nzima kwa ajili ya kufungua akaunti na kuanza kuwawekekea akiba. Aliwataka wazazi pia kuwafundisha watoto kujiwekea akiba wenyewe katika akaunti zao jambo litakalosaidia kuwajenga katika kuweka akiba na matumizi sahihi ya fedha.

Lasway alisema Benki hiyo imerahisisha kwa kiasi kikubwa utoaji wa huduma zake kwa kuwekeza katika mifumo ya kidijitali inayowawezesha wateja kupata huduma popote pale walipo na kwa urahisi. 

“Kupitia njia hizi za kidijitali kama SimBanking, SimAccount, Internet Banking mzazi anaweza kuweka fedha moja kwa moja katika akaunti ya Junior Jumbo ya mtoto bila ya kutembelea tawini,” alisema Lasway huku akibainisha wateja pia wanaweza kuweka fedha katika akaunti kwa kuhamisha moja kwa moja kutoka katika mitandandao ya simu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad