WAZIRI
wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ameutaka uongozi wa shirikisho
la soka Zanzibar (ZFF) kuacha tabia ya kutengeneza makundi ili kuepuka
kuwafarakanisha wachezaji na kusababisha migogoro katika vilabu vya soka
hilo.
"Ondoeni kabisa tabia ya kutengeneza makundi yatavunja sana..."
Amesema suala hilo ni chachu ya kujenga chuki na migongano baina yao
hali inayopelekea shirikisho la soka Zanzibar kushuka na kuiweka nchi
katika nafasi mbaya kisoka.
Amewasisitiza sana suala la kufuata katiba
na kanuni zilizoundwa katika kuendesha shughuli zote za mpira wa miguu
ili kuepusha kufanya maamuzi ya ubaguzi, upendeleo na kupelekea
sitonfahamu kwa uongozi wa ZFF na vilabu vya mpira.
Kwa upande mwengine
amewasisitiza kuaminiana, kupendana, kushirikiana, kujielewa na
kuwajibika ipasavyo ili kuweza kufanikiwa kurejesha haiba ya soka la
Zanzibar Aidha Mhe. Tabia ameahidi kushirikiana nao kikamilifu kwa
ushauri, kutafuta wadhamini, kupanga na kutekeleza mikakati itakayokuza
soka la Zanzibar.
Waziri
wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (Zanzibar), Tabia Mwita akizungumza wakati akiteua uongozi wa shirikisho
la soka Zanzibar (ZFF) leo.
No comments:
Post a Comment