Na Pamela Mollel Michuzi blog,ARUSHA
MBUNGE
wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo amesema atahakikisha watu wote wenye
ulemavu 565 katika Jiji la Arusha atawapatia viti mwendo 100 na
kuwapatia matibabu kwa kupindi cha miaka mitano kupitia Mfuko wa Bima
ya Afya (NHIF).
Aidha amesema atachimba visima vya maji kwenye
soko kuu la Arusha,Samunge,Kijenge na kwa kuanza ameshachimba kisima
katika soko la Kilombero.
Akizungumza ofisini kwake leo jijini
Arusha na Waandishi wa Habari,Gambo alisema mbali na masoko hayo pia
atachimba visima kwenye shule zenye uhitaji wa maji ili wanafunzi wapate
huduma hiyo bila kuhangaika.
"Lakini katika uongozi wangu
nitaweka nguvu kubwa katika kutatua kero za wafanyakazi wa viwandani na
kwa kuanza nitafanya ziara ya siku nne kwenye kiwanda cha A to
Z,Sunflug,Lothia na Tanfoam na nitaongozana na wataamu toka Idara ya
kazi, Osha,NSSF,PSSF,Mfuko wa Fidia kwa wafanyaka pamoja na viongozi wa
vyama vya wafanyakazi,"alisema Gambo.
Alisema ziara hiyo
imetokana na kupokea malalamiko mengi ya wafanyakazi hao wakati
alipotembelea kwenye viwanda hivyo kuomba kura wakati wa kampeni za
uchaguzi mkuu na kuahidi kuzifanyia kazi mara baada ya kuchaguliwa.
Aidha
alisema waajiri wengi hawatoi mikataba kwa wafanyakazi wao,lakini
viongozi wa serikali wanapowatembelea huonyeshwa mikataba hewa,huku
wafanyakazi wakiendelea kuteseka.
Kuhusu ukusanyaji wa taka
katika jiji hilo alisema amepokea malalamiko mengi kutoka kwa wnaanchi
za kutozwa gharama kubwa za uzoaji wa taka na kwamba atajenga hoja
kwenye barasa la madiwani ili gharama zipunguzwe.
Kwa upande wa
sekta binafsi amepokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya wawekezaji
kunyimwa vibali vya kuajiri raia wa kigeni kwa madai kwamba kuna
watanzania wenye uwezo wa kufanya kazi hizo.
Aidha kwa upande wa
mikopo Gambo alisema amefanya uchunguzi na kubaini vikundi vya watu
wenye ulemavu,vijana na wanawake kila kundi linapewa mikopo na matokeo
yake kila mtu anakwenda kufanya biashara yake na ikitokea mmoja wao
ameshindwa kurejesha kikundi kizima kinachukuliwa hatua kitu ambacho
siyo sahihi.
Alisema atalijengea hoja bungeni ili kuwe na
utaratibu wa kukopesha mtu mmoja mmoja na sio kikundi ili kila mtu abebe
mzigo wake mwenyewe pale atakaposhindwa kurejesha
Mbunge
wa Jimbo la Arusha mjini kupitia chama Cha Mapinduzi Mrisho Gambo
akizungumza na vyombo vya habari leo katika ofisi ya Mbunge
No comments:
Post a Comment