HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 18, 2020

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA VIWANDA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA BEI YA SARUJI

 

 

Naibu katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara  Bw.Ludovick J.Nduhiye  akisikiliza kwa makini maelezo  kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa  Kampuni ya Portland Cement Tanzania Bw.  Alfonso Velez kuhusu Changamoto ya upandaji bei cement na  jinsi  Kampuni  hiyo inayozalisha cement ya Twiga ilivyojipanga kupunguza usafirishaji wa cement nje ya nchi ili kukabiliana na changamoto iliyopo. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi za kampuni hiyo , Wazo Jijini Dar es salaam tarehe 16/11/2020 ikiwa ni muendelezo wa ziara ya kutembelea Viwanda na wasambazaji wa Cement ili  kufanya tathimini ya changamoto hiyo na jinsi ya kukabiliana nayo.
Mkurugenzi Mkuu wa  Kampuni ya Portland Cement Tanzania (TPCCL)  Alfonso Velez akitoa maelezo kwa Naibu katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Ludovick J. Nduhiye kuhusu jinsi    Kampuni  hiyo inayozalisha cement ya Twiga ilivyojipanga kukabiliana na changamoto hiyo , Wapili kushoto ni  Bw. Richard Magoda meneja wa Mazingira wa TPCCL na  wa pili  kulia ni Bw. Christopher Nassari Kaimu Mkurugenzi Idara ya Biashara  Wizara ya Viwanda na Biashara . Mazungumzo hayoyalifanyika katika ofisi za kampuni hiyo, Wazo Jijini Dar es salaam tarehe 16/11/2020 ikiwa ni muendelezo wa ziara ya kutembelea Viwanda na wasambazaji wa Cement ili  kufanya tathimini ya changamoto hiyo na jinsi ya kukabiliana nayo.
Naibu katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Ludovick J. Nduhiye akizungumza na  Katibu Tawala wa Mkoa Mkuu wa Dar es salaam , Paulo Mshimo Makanza Ofisini kwake  Jijini Dar es salaam tarehe 16/11/2020 kuhusu changamoto ya upandaji bei cement na jinsi ya kukabiliana nayo. Huu ni muendelezo wa ziara inayofanywa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda katika kufanya tathimini  ya Uapandaji bei Cement na Vifaa vya ujenzi.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad