Naibu
katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Bw.Ludovick J.Nduhiye
akisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni
ya Portland Cement Tanzania Bw. Alfonso Velez kuhusu Changamoto ya
upandaji bei cement na jinsi Kampuni hiyo inayozalisha cement ya
Twiga ilivyojipanga kupunguza usafirishaji wa cement nje ya nchi ili
kukabiliana na changamoto iliyopo. Mazungumzo hayo yalifanyika katika
ofisi za kampuni hiyo , Wazo Jijini Dar es salaam tarehe 16/11/2020
ikiwa ni muendelezo wa ziara ya kutembelea Viwanda na wasambazaji wa
Cement ili kufanya tathimini ya changamoto hiyo na jinsi ya kukabiliana
nayo.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kampuni ya Portland Cement Tanzania (TPCCL) Alfonso Velez
akitoa maelezo kwa Naibu katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara
Ludovick J. Nduhiye kuhusu jinsi Kampuni hiyo inayozalisha cement ya
Twiga ilivyojipanga kukabiliana na changamoto hiyo , Wapili kushoto ni
Bw. Richard Magoda meneja wa Mazingira wa TPCCL na wa pili kulia ni
Bw. Christopher Nassari Kaimu Mkurugenzi Idara ya Biashara Wizara ya
Viwanda na Biashara . Mazungumzo hayoyalifanyika katika ofisi za kampuni
hiyo, Wazo Jijini Dar es salaam tarehe 16/11/2020 ikiwa ni muendelezo
wa ziara ya kutembelea Viwanda na wasambazaji wa Cement ili kufanya
tathimini ya changamoto hiyo na jinsi ya kukabiliana nayo.
Naibu
katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Ludovick J. Nduhiye
akizungumza na Katibu Tawala wa Mkoa Mkuu wa Dar es salaam , Paulo
Mshimo Makanza Ofisini kwake Jijini Dar es salaam tarehe 16/11/2020
kuhusu changamoto ya upandaji bei cement na jinsi ya kukabiliana nayo.
Huu ni muendelezo wa ziara inayofanywa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda katika kufanya tathimini ya Uapandaji bei Cement na Vifaa vya
ujenzi.
No comments:
Post a Comment