ECOBANK
Tanzania imetoa msaada wa vifaa vya kupima ugonjwa wa kisukari katika
Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya
mkakati wao wa kutenga siku maalum kusaidia jamii.
Kwa
mujibu wa Ecobank ni kwamba miaka mitatu mfululizo Ecobank imekuwa
ikitenga siku kusiadia jamii kwa kutatua changamoto zao mbalimbali za
kimaisha.
Taarifa
ya Ecobank kwa vyombo vya habari imeeleza mwaka huu wamejikita katika
kusaia kuelimisha na kusaidia kupunguza janga la ugonjwa wa Kisukari kwa
kushirikiana na NDC alliances kwa kuendesha kongamano na mjadala
kuelimisha watu jinsi ya kula vizuri.
Pia
kufanya mazoezi na kupima afya zao mara kwa mara ilikuweza kujiepusha
na janga hilo la ugonjwa wa Kisukari. Kongamano liliendeshwa kwa
njianya mtandao Kwa kuzingatia janga la Corona duniani.
"Kwa
hapa Tanzania, Ecobank imeshiriki siku ya Sukari duniani kwa kupima
wafanyakazi wao, Sukari, Blood pressure na uzito. Zoezi hili
liliendeshwa na kampuni ya udalali wa huduma za bima (ARIS) pamoja Jubelee insurance.
"Ecobank
Tanzania pia imetoa msaada wa vifaa vya kupimia ugonjwa wa Kisukari kwa
hospitali ya Mwananyamala. Vifaa kama vile, Glucometers, BP machines na
vifaa vya kupimia uzito (weighing machines) vilikabidhiwa kwa uongozi
wa hospitali ya Mwananyamala,"amesema.
Akipokea
vifaa hivyo Dk. Mfawidhi Dk Daniel katika Hospitali ya Mwananyamala
ameishukuru benk hiyo na kwamba vifaa hivyo vitaisdia kwani vimetolewa
wakati muafaka."Vifaa hivi vitasaidia kutakua tatizo ka uhaba wa vifaa
vya kupimia sukari hopitalini hapo."
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya Ecobank Tanzania, Charles
Asiedu(kushoto) akizungumza na wafanyakazi wa hosptali ya Mwananyamala
pamoja na wafanyakazi wa Benki ya Ecobank Tanzania wakati wa kutoa
msaada wa vifaa tiba kwenye hospitali ya Mwananyamala iliyopo kwatika
wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam kwenye maadhimisho ya siku ya
Benki ya Ecobank .
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya Ecobank Tanzania, Charles Asiedu(kushoto)
akimkabidhi msaada wa vifaa tiba Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya
Mwananyamala, Dkt. Daniel Nkungu(kulia) kwenye
hospitali ya Mwananyamala iliyopo kwatika wilaya ya Kinondoni jijini
Dar es Salaam kwenye maadhimisho ya siku ya Benki ya Ecobank.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mwananyamala, Dkt. Daniel Nkungu
akitoa neno la shukran kwa uongozi wa Ecobank Tanzania mara baada ya
kupokea msaada wa vifaa tiba kwa ajili ya hospitali ya Mwananyamala
iliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam
Wafanyakazi
wa Benki ya Ecobank Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja na
wafanyakazi wa hospitali ya mwananyamala mara baada ya kumalizika kwa
zoezi la kutoa msaada wa vifaa tiba katika hospitali hiyo
Wafanyakazi
wa Ecobank Tanzania wakishiriki siku ya Sukari duniani kwa kupima afya
zao kama kupima Sukari, Blood pressure na uzito. Zoezi hili liliendeshwa
na kampuni ya udalali wa huduma za bima (ARIS) pamoja Jubelee insurance.
No comments:
Post a Comment