HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 18, 2020

CSI TANZANIA WAAHIDI KUENDELEA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA TAASISI YA DORIS MOLLEL FOUNDATION KATIKA KUSAIDIA WATOTO WANAOZALIWA KABLA YA WAKATI

 
 
Meneja wa Programu za Vijana Shirika la Childbirth Survival International(CSI) CSI, Ester Mpanda akizungumza kuhusu CSI Tanzania inavyoshirikiana na Doris Mollel Foundation wakati wa maadhimisho Siku ya Mtoto Njiti Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Novemba 17 ya kila mwaka yaliyofanyika katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam
 
Na Said Mwishehe, Michuzi TV
SHIRIKA la Childbirth Survival International(CSI) lenye makao makuu yake nchini Marekani limeendelea kuwasisitiza Watanzania na wadau wengine nchini kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation katika kusaidia watoto njiti kwani malezi yao yamekuwa na  changamoto nyingi.

Aidha limesema linashukuru kwa taasisi hiyo ya Doris Mollel Foundation kukubali kufanya kazi na wao kwa kuleta watu pamoja kuhusu masuala yanayohusu afya ya mama na mtoto na kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Novemba 17 ya kila mwaka.

Akizungumza jijini Dar es Salaam mbele ya viongozi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, madaktari, wauguzi na wadau wengine, Meneja wa Programu za Vijana kutoka CSI Ester Mpanda amesema kuwa karibu  na Doris kumewasaidia kujua watoto njiti wanavyopitia changamoto nyingi katika masuala ya afya kutokana na kuzaliwa kabla ya wakati na kwamba vifo vingi vya watoto chini ya miaka mitano ni vifo vya watoto njiti.

Katika kuadhimisha siku hiyo ya Mtoto Njiti Duniani ,Taasisi ya Doris Mollel Foundation iliamua kuandaa sherehe maalum iliyoambana na kuwasha taa za zambarau katika wodi ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambapo CSI ni miongoni mwa wadau muhimu waliohuduria tukio hilo.

Wakati wa sherehe hizo ,pia viongozi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto, Katibu wa Itikadi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), madaktari, wauguzi na wadau wengine mbalimbali wameungana na Doris Mollel Foundation kuadhimisha siku hiyo.
"Shirika letu la CSI ambalo makao makuu yake yapo nchini Marekani tumejikita zaidi katika kuangalia afya ya mama na mtoto wakati akiwa amebeba mimba na kujifungua ,tuna programu ambazo zinawasidia wamama kujua viashiria hatarishi.

"Pia tumekuwa tukitoa elimu inayozungumzia mambo muhimu wanayopaswa kuzingatiwa kwa mama aliyebeba mimba ili kubaki salama yeye na watoto watakawaozaa, tumekuwa tukisaidia vifaa kwa kujifungulia.CSI tunazo programu ya wasichana ambayo inayompa elimu ya kujitambua, kujielewa na  hasa masuala ya kujihusisha na ngono kabla ya umri rasmi , yote hiyo ni kumfanya awe makini na kuanza kutambua mapema viashiria hatarishi kuhusu masuala ya uzazi,"amesema Mpanda.

"CSI tunawashukuru wote ambao wameungana na Doris kwa ajili ya kumsapoti, tunaamini kumsapoti Doris ndio ni kutusapoti na sisi, huu ni mwaka watatu tunafanya kazi na Doris ambaye amekuwa na moyo wa upendo dhidi ya watoto njiti.
"Hivyo shirika letu ambalo limejikita katika kuhakikisha tunapunguza vifo vya  mama na mtoto, tunatoa rai kwa jamii yote kuendelea kumsaidia Doris kwani amebeba mzigo mkubwa sana na anataka watu wote wajue umuhimu wa siku ya leo inayotoa  nafasi ya kutambua jinsi mtoto njiti anavyopata tabu,"amesema Mpanda.

Ametumia nafasi hiyo kwa niaba ya CSI kuwashukuru na kutambua kazi kubwa na nzuri ambayo inafanywa na madaktari na wauguzi kote nchini ambao wamekuwa wakitumia muda mwingi kuangalia maisha ya mama na mtoto na hasa kuona wanabaki salama.

Amekumbusha CSI ni shirika ambalo linajihusisha na afya ya mama na mtoto hasa katika kudhibiti vifo vitokanavyo na uzazi kwa mama na mtoto wakati wa kujifungua."Tuko tena hapa jioni ya leo kwasababu ya kuthibitisha kwa vitendo jinsi CSI tunavyomuunga mkono Doris na tutaendelea."

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad