Baadhi
ya Washiriki wa kikao Cha wadau wa uchaguzi mkoa wa Arusha wakifuatilia
mjadala ulikuwa ukiendelea,mbele yao ni Frimin Miku mwezeshaji katika
kikao hicho
Kaimu Shekhe mkoa wa Arusha akichangia mada katika kikao Cha wadau wa uchaguzi mkoa wa Arusha kilichoandaliwa na TAWLA
Baadhi
ya Washiriki wa kikao Cha wadau wa uchaguzi mkoa wa Arusha wakifuatilia
mjadala ulikuwa ukiendelea,mbele yao ni Frimin Miku mwezeshaji
katika kikao hicho
Wa
kwanza Kushoto ndugu Mabula kutoka katika ofisi ya Mkuu wa mkoa
wa Arusha akiwa na baadhi ya Washiriki wa kikao Cha wadau wa uchaguzi
mkoa wa Arusha wakifuatilia mjadala ulikuwa ukiendelea,mbele yao ni
Frimin Miku mwezeshaji katika kikao hicho
Baadhi
ya Washiriki wa kikao Cha wadau wa uchaguzi mkoa wa Arusha wakifuatilia
mjadala ulikuwa ukiendelea,mbele yao ni Frimin Miku mwezeshaji katika
kikao hichoWatanzania
wametakiwa kuhakikisha wanafuata kanuni taratibu zilizowekwa na tume ya
Uchaguzi kwa lengo kutochochea vurugu wakati wote wa zoezi la upigaji
wa kura.
Aidha tume ya Uchaguzi iwe muangalizi wa misingi ya Demokrasia wakati wote wa uchaguzi Ili kuendana na Uchaguzi huru na haki.
Hayo
yamesemwa na Chama Cha wanasheria wanawake Tanzania (TAWLA) katika
kikao Cha wadau wa uchaguzi kutoka Asasi za Serikali na zile za Kiraia
mkoa wa Arusha kwa lengo la kujadili uendeshaji wa uchaguzi na wajibu wa
kila mdau.
Mratibu
wa TAWLA mkoa wa Arusha Happyness Mfinanga , alisema kuwa Dira ni
kuhamasisha jamii ,kulinda na,kutetea wanawake kwa kutoa Elimu juu ya
ubaguzi wa Kijinsia ,ambapo katika upigaji kura kwaajili ya kuchagua
Viongozi na wanakwake pia wapo hivyo lazima waheshimiwe.
Mfinanga alisema
kuwa dhumuni lao ni kuendelea wanawake Kama vinara katika kutetea,
kulinda haki za wanawake ,na utawala bora kupitia Elimu ya kisheria huku
alisema itikafi yao ni uwajibikaji, uadilifu,utofauti,kujitolea na
utaalam.
Akizungumza
mwezeshaji wa mjadala huo Firmin Miku aliwaongoza wadau hao,katika
kuangalia ya Uchaguzi,siku ya Uchaguzi na baada ya Uchaguzi jinsi ya
kuweza kufanya Uchaguzi wa kidemokrasia
Sambamba
na hayo Waliweza kujadili kwa kina juu ya wajibu wa kila mdau, katika
Uchaguzi mkuu Ikiwemo Tume ya Uchaguzi, kwani ndiyo yenye jukumu la
kutangaza matokeo ya Uchaguzi haswa ya Urais.
Aidha
katika ngazi za majimbo wakiwemo wasimamizi wa uchaguzi kuratibu
upatikanaji wa rasilimali fedha, kwaajili ya kukamilisha na kusimama
taratibu zote za Uchaguzi ,sambamba na kuhakikisha Uchaguzi kunakwenda
Kama ulivyopangwa.
Akichangia
mada katika kikao hicho kutoka Taasisi ya Women and Children Vision
(WOCHIVI) Faith Swai ,alisema ufike wakati vyombo vya Ulinzi na Usalama
vipatiwe Elimu, juu ya Jinsia Ili hata wanapomkamata mtuhumiwa mwanamke,
watambue namna ya kukumfikisha eneo husika bila kumdhalilisha
"Wakati
mwingine ukiwaona baadhi ya Askari wanavyowakamata watuhumiwa mwanamke,
ukweli inaumiza hivyo tunawaomba wahusika mtusaidie kutoa Elimu juu ya
Jambo hilo "Alisema Faith
Swai aliweza
kuongeza kwa kusema kuwa ufike wakati vyama vya siasa ,vitoe elimu juu
ya matumizi ya lugha njema wawapo majukwaa ya siasa ,bila kuwadhalilisha
wanawake, katika Kampeni zao.
Chama
Cha Wanasheria nchini Tanzania (TAWLA) kiliwataka wadau hao, Kutambua
kuwa kupiga kura kwa mwananchi aliyekidhi vigezo, ni haki yake ya Msingi
hivyo ifikapo tarehe 28/10/2020 ni vyema wakapige kura kwaajili ya
kumchagua viongozi wanaomtaka, kwajili ya maendeleo ya Taifa lao.
No comments:
Post a Comment