Mgombea
Ubunge wa Jimbo la Mbeya mjini kwa tiketi ya CCM Dr. Tulia Ackson
ameshiriki kampeni za kunadi sera za chama chake katika kata ya Iganzo
jijini humo ambapo amewataka Wananchi kupiga kura zote za kishindo na
Chama Cha Mapinduzi itapofika siku ya October 28, 2020 ili wayapate
maendeleo ya kweli kupitia Serikali ya awamu ya tano.
Dr.
Tulia ambaye alikuwa ameambatana na baadhi ya Viongozi wa Chama Cha
Mapinduzi Wilaya pamoja na mchekeshaji Emmanuel Mathias maarufu kama MC
PILIPILI amesema>>>
“Ndugu
zangu kama ambavyo nasisitiza siku zote kwamba CCM tuna hoja na wenzetu
wana vihoja, chagueni viongozi wanaotatua changamoto zenu na sio
wanaotoa malalamiko kila kukicha. Hapa Mbeya tunataka Mbunge wa
kujiongeza hivyo basi safari hii tusifanye makossa katika kuchagua” -Dr.
Tulia Ackson
“Kwenye
eneo la afya mimi nilishakuja hapa kwenye zhanati Iganzo na nikaleta
kitanda cha kujifungulia wakinamama na mashuka, sisi tunataka ukija hapa
Iganzo usitupe stori tu bali tueleze umefanya nini. Kama hatukuwahi
kukuona kwenye shule zetu, hatukukuona kwenye zahanati basi safari hii
Mbeya mjini tutachagua mtu tuliyekata naye kuni ndio tutakayeota naye
moto”-Dr. Tulia Ackson
“Sisi
ni watu wa kazi na watu wa kujiongeza, tunaposema hivyo tunamaanisha
kweli kweli. Na leo ni vile muda hautoshi tungewaleta hapa baadhi ya
wazee hapa Mbeya jiji ambao kwa kupitia kwangu kama mbunge wa Connection
tumewasaidia bima za afya bure kwa kupitia Tulia Trust, acha hilo tu
kwenye uwezeshaji kiuchumi tumewawezesha mikopo ya riba nafuu
Wakinamama, Vijana na hata wazee. Sasa huo ni mwanzo tu chagueni Tulia
awe Mbunge wenu mjionee makubwa mengine”-Dr. Tulia Ackson
No comments:
Post a Comment