Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara na mgeni 
rasmi akizinduwa maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika katika 
Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, Mkoani Dodoma leo yalioandaliwa na 
Mtandao wa Elimu Tanzania (TENMET). Kulia Mratibu wa Taifa wa TENMET, 
Bw. Ochola Wayoga.
Mratibu wa Taifa wa TENMET, Bw. Ochola Wayoga (kulia) akizungumza katika maadhimisho hayo.
Kutoka kushoto ni Afisa Elimu Sekondari Chemba, Valentine 
Christopher na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara 
wakiwa meza kuu.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara na mgeni 
rasmi katika maadhimisho ya Juma la Elimu akipokea begi lenye mchapisho 
ya maadhimisho hayo kutoka kwa Mratibu wa Taifa wa TENMET, Bw. Ochola 
Wayoga, alipotembelea banda la TENMENT kwenye maadhimisho hayo 
yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, Mkoani Dodoma leo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara (kulia) 
akipata maelezo alipotembelea Banda la TENMET katika maadhimisho ya Juma
 la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, 
mkoani Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara (kulia) 
akipata maelezo alipotembelea Banda la TENMET katika maadhimisho ya Juma
 la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, 
mkoani Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara (kulia) 
akipata maelezo alipotembelea Banda la UWEZO katika maadhimisho ya Juma 
la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, mkoani
 Dodoma. Katikati ni Mratibu wa Uwezo Mkoa wa Dodoma, Nason Nason 
akifuatilia,
Mratibu wa Uwezo Mkoa wa Dodoma, Nason Nason (katikati) 
akimuonesha moja ya machapisho yao Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, 
Mh. Mwita Waitara (kulia) alipotembelea Banda la UWEZO katika 
maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya 
Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara (kushoto) 
akipokea maandamano kwenye maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika 
katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara (kushoto) 
akipokea maandamano kwenye maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika 
katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Bendi ya matarumbeta ikiongoza msafara wa maandamano kwenye 
maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya 
Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Maandamano ya wanafunzi kwenye maadhimisho ya Juma la Elimu 
yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Maandamano ya wanafunzi wakiwa na mabango ya jumbe mbalimbali 
kwenye maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya 
Shule ya Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Maandamano ya wanafunzi wakiwa na mabango ya jumbe mbalimbali 
kwenye maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya 
Shule ya Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Maadhimisho ya Juma la Elimu yanayofanyika wilayani Chemba, mkoani Dodoma.
Maandamano ya wanafunzi kwenye maadhimisho ya Juma la Elimu 
yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara 
alipotembelea Banda la Watoto Wetu Tunu Yetu-Dodoma katika maadhimisho 
ya Juma la Elimu yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi 
Chemba, mkoani Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara 
alipotembelea Banda la HakiElimu katika maadhimisho ya Juma la Elimu 
yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, mkoani Dodoma.
Na Joachim Mushi, Chemba
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mwita Waitara ameupongeza 
Mtandao wa Elimu Tanzania (TENMET) kwa jitihada inazozifanya pamoja na 
wanachama wake kwa kuiunga mkono Serikali hasa katika sekta ya elimu 
kushirikiana tutatua baadhi ya changamoto za elimu.
Naibu Waziri Waitara ameyasema hayo leo wilayani Chemba alipokuwa 
akizinduwa maadhimisho ya Juma la Elimu mwaka huu yanayofanyika katika 
Viwanja vya Shule ya Msingi Chemba, ikiwa ni kuleta chachu ya 
uwajibikaji kwenye sekt ya elimu kwa familia za wafugaji na jamii.
Alisema Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Pombe 
Magufuli ilipoingia madarakani ilibaini kuna kundi ambalo la watu 
wasiojiweza walikosa elimu kutokana na changamoto mbalimbali za 
uchangiaji, hivyo iliamua kuja na mfumo wa kutoa elimu bila ada. 
"...Kulikuwa kuna watoto walishindwa kwenda shule, hivyo Rais John 
Pombe Magufuli akaamua elimu kuanzia ya awali mpaka kidato cha nne iwe 
bure, kwa maana kwamba elimu bila ada. Hii ndio inaitwa elimu msingi 
bila malipo. Maamuzi hayo yalipata mafanikio makubwa kwani iliongeza 
uandikishaji na ufaulu,"
"..Uandikishaji ulipanda kutoka watoto milioni 10 hadi milioni 12 
hili ni jambo kubwa na tunampongeza mheshimiwa Rais Magufuli kwa kuliona
 hilo, maana wapo vijana ambao walikuwa mtaani lakini sasa walienda 
shule na kuendelea na masomo kidato cha nne hadi cha sita, na pia 
wengine wameenda hadi vyuo," alisema Waitara na kuongez kuwa Serikali 
inatumika takribani bilioni 24 kila mwaka kwa ajili ya kuwezesha mpango 
huo wa serikali. 
Aliongeza kuwa baadaye mwongozo ulitoka wa waraka namba tatu wa mwaka
 2016 ulioonesha namna ambavyo jamii inashirikishwa kuchangia kutatua 
changamoto ndogondogo kwenye elimu ili kuboresha zaidi. 
Alisema Serikali licha ya kutoa elimu bila malipo haijafanikiwa kutoa
 chakula kwa shule zote, hivyo imeelekeza wazazi wanaweza kujipanga na 
kuchangia chakula ili mtoto aweze kujifunza huku akipata mlo jambo 
ambalo linaweza hata kumfanya akaweza kushiriki kikamilifu kupokea 
mafunzo toka kwa walimu. 
Pamoja na hayo, alibainisha kumekuwa na wazazi ambao wamekuwa 
hawaupokei vizuri mpango huo wa kuchangi na ndio maana yapo mashirika 
yanajitolea kusaidia suala hilo, na hata nyie (TENMENT) nimeona 
mkihamasisha wazazi kujitokeza kuchangia ili kupunguza changamoto katika
 sekta hii. Lazima tuelewe kuwa hawa watoto ni wakwetu, shule ni za 
kwetu na nijukumu la jamii kusaidia watoto wetu.
Aidha alisema jambo lingine ambalo linajitokeza kwa sasa ni wazazi 
kujiweka pembeni kwenye ufuatiliaji taarifa za mtoto wake awapo shuleni,
 wapo wazazi ambao wakishapeleka mtoto shule wao hujivua kabisa 
kufuatilia taarifa za mtoto na mwishoni wanajitokeza kumlaumu mwalimu 
pale mtoto anapofeli mtihani wa mwisho hili sio sawa wazazi lazima 
tubadilike tufuatilie elimu ya watoto wetu.
Naye Mratibu wa Taifa wa TENMET, Bw. Ochola Wayoga alisema 
maadhimisho ya mwaka huu yamelenga kuhamasisha uelewa wa jamii juu ya 
haki ya kupata elimu, kuongeza uhamasishaji kwa jamii juu ya uwajibikaji
 wa pamoja wa elimu na kuhamasisha Serikali kuzingatia na watoto wenye 
uhitaji, ikiwemo miundombinu ya shule, vifaa vya mafunzo na mafunzo ya 
ualimu.
Amebainisha kuwa kutokana na changamoto zilizopo katika sekta ya 
elimu, Serikali haipaswi kuachiwa kila kitu hivyo wadau wanakila sababu 
ya kujitokeza na kushiriki kuchangia masuala mbalimbali kwenye sekta 
hiyo kusaidia kutatua baadhi ya changamoto. 
Katika maadhimisho hayo yalioambatana na maonesho ya shughuli za 
wanachama wa TENMET, yatashirikisha uchangiaji wa gharama za ujenzi wa 
bweni la wanafunzi katika Shule ya Sekondari Kwamtoro iliyopo Wilaya ya 
Chemba. 
Maadhimisho hayo yanaofikia tamati Agosti 21 yataambatana na mijadala
 mbalimbali, midahalo, ushiriki katika utoaji wa elimu kupitia vyombo 
vya habari juu ya masuala anuai ya elimu na changamoto zake kwa ujumla.
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment