Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa leo Agosti 25, 2020 ametangazwa na Tume ya Taifa
ya Uchaguzi (NEC) KUPITIA msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya
Ruangwa kupita bila kupingwa katika nafasi ya Ubunge wa Jimbo la
Ruangwa.
Akitangaza
matokeo hayo kwenye viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya
Ruangwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Frank Chonya amesema
Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Majaliwa ndiye pekee
aliyekidhi vigezo vilivyowekwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kumfanya
kupita bila kupingwa.
Akizungumza
baada ya kutangazwa kuwa amepita bila kupingwa, Mheshimiwa Majaliwa
amesema anawashukuru wanaCCM, Viongozi na wanachama wa vyama
rafiki na wana Ruangwa kwa ujumla kwa heshima waliyompatia na
kumwezesha kupita bila kupingwa.
“Sisi
wanaRuangwa wote bila kujali siasa zetu tunajua tulikotoka na wilaya
hiitunajua changamoto tulizonazo kwenye wilaya hii lakini tunajua hatua
tuliyoifikia sasa hivi na kauli zenu zilikuwa zinaangalia tunakokwenda
na uwezekano wa kutatua changamoto huko mbele na ndiyo kwa sababu basi
mwakilishi huyu tumpe nafasi nyingine tena aendelee”.
Aidha,
Mheshimiwa Majaliwa ameahidi kuwa ataendelea kuwa mtumishi wa
wanaRuangwa, kuendelea kuwa mhudumu wao, kuwa mwakilishi wao katika
maeneo mbalimbali na ataendelea kuwasemea.
“Ahadi
yangu ni kuwatumikia wote bila kujali vyama vyenu vya siasa, makabila
yenu, maeneo mnayotoka wala uwezo wenu. Ninyi wote nawaona kuwa ni
wazazi wangu, mama zangu, baba zangu, kaka zangu, dada zangu lakini pia
wadogo zangu”.
Pia
Waziri Mkuu amesema kuwa Ruangwa imepata heshima kubwa kutoka kwa Rais
Dkt. John Pombe Magufuli ya kumsaidia kazi ambayo pia iliwezesha
kutatua matatizo mbalimbali katika wilaya ya Ruangwa.
No comments:
Post a Comment