HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 25, 2020

MAJALIWA APITA BILA KUPINGWA JIMBO LA RUANGWA

 

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Agosti 25, 2020 ametangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) KUPITIA msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kupita bila kupingwa katika nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Ruangwa.

Akitangaza matokeo hayo kwenye viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Frank Chonya amesema Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Majaliwa ndiye pekee aliyekidhi vigezo vilivyowekwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kumfanya kupita bila kupingwa.

Akizungumza baada ya kutangazwa kuwa amepita bila kupingwa, Mheshimiwa Majaliwa amesema anawashukuru  wanaCCM, Viongozi na  wanachama wa vyama rafiki  na wana Ruangwa kwa ujumla  kwa heshima waliyompatia na kumwezesha kupita bila kupingwa.

“Sisi wanaRuangwa  wote bila kujali siasa zetu tunajua tulikotoka na wilaya hiitunajua changamoto tulizonazo kwenye wilaya hii lakini tunajua hatua tuliyoifikia sasa hivi  na kauli zenu zilikuwa zinaangalia tunakokwenda na uwezekano wa kutatua changamoto huko mbele na ndiyo kwa sababu basi mwakilishi huyu tumpe nafasi nyingine tena aendelee”.

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ameahidi kuwa ataendelea kuwa mtumishi wa wanaRuangwa, kuendelea kuwa mhudumu wao, kuwa mwakilishi wao katika maeneo mbalimbali na ataendelea kuwasemea.

“Ahadi yangu ni kuwatumikia wote bila kujali vyama vyenu vya siasa, makabila yenu, maeneo mnayotoka wala uwezo wenu.  Ninyi wote nawaona kuwa ni wazazi wangu, mama zangu, baba zangu, kaka zangu, dada zangu lakini pia wadogo zangu”.

Pia Waziri Mkuu amesema kuwa Ruangwa imepata heshima kubwa kutoka kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kumsaidia kazi  ambayo pia iliwezesha kutatua matatizo mbalimbali katika wilaya ya Ruangwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad