HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 31, 2020

CCM YAWAJIA JUU WAPINZANI WAO, YAMTAKA MZEE YULE KUACHA KUTAJA VIONGOZI WAKE

 

 Katibu wa Itikadi ya Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humprey Polepole (katikati) akisisitiza jambo wakati akitangaza majina ya wagombea wa nafasi ya Uwakilishi kwa Zanzibar yaliyopitishwa leo na Kamati Kuu ya Chama hicho, jijini Dodoma. wengine pichani ni Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM.
Na Said Mwishehe, Michuzi TV- Dodoma

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimetuma salamu kwa vyama vya upinzani kwa kuwataka kuacha chokochoko na wasioutakia mema nchi yetu huku kikitoa rai kwa wapinzani kuacha kutaja taja majina ya viongozi wao.

Akizungumza leo jijini Dodoma ,Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Humphery Polepole amesema kabla ya kusoma majina ya wagombea waliopitishwa kugombea ujumbe w baraza la wawakilishi ni vema kwanza akazungumzia mwenendo wa kampeni unavyoendelea kule Zanzibar na siasa zake.

Hivyo amesema kwamba "tungependa kuujulisha umma ya kwamba Chama Cha Mapinduzi tuko vizuri mno kwa maana ya wana CCM kule , wananchi wa kawaida kule, ambao wanatuelewa vizuri mno , wameupokea vizuri zaidi uteuzi wa ndugu yetu Hussein Mwinyi ambaye mpaka sasa hivi tumesema usikimbie.

",Sasa hivi anapiga jaramba ya kujiweka sawasawa na sisi tunajua yule ni kijana ,tena  kijana ambaye kwenye uongozi ni bado ana nguvu zake ambazo wanzazibar wanaweza kuzitumia kwa maslahi mapana ya Zanzibar kwa muda huu.Lakini tunajua tunao mahasimu wetu ambao hawatatutakii mema na leo sikutaka kumsema yoyote katika nyumba hii kubwa ya CCM.

"Lakini nataka kutoa rai mzee yule (ambaye hakumtaja jina) aache kutaja majina ya viongozi wetu, aache na leo nimetoa heshima kubwa , nimeambatana hapa na wajumbe wenzangu wa Halmashauri Kuu Taifa Bara na Zanzibar ili haya ambayo ninawaeleza ifahamike ndio msimamo wa Chama chetu,"amesema Polepole.

Amesisitiza ni vema akaachana na anajua Chama Cha Mapinduzi wamepiga hatua na itakuwa ngumu kwa vyama vingine kupiga siasa ya kueleweka ,wajipange sio kutengeneza hoja ya kubumba bumba zisizo na mashiko.

",Nimehuzunika sana mzee yule kwasababu anasema uongo kabisa tena hadharani na sina hakika huenda anatafuta namna tumshitaki ili apate kiki kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu, hakuna kitu kingine anachotaka zaidi ya kuvuta hisia za watu.

"Anataka kutengeneza kitu hivi, kutengeneza umaarufu sisi hatutafanya hivyo lakini tunamuonya afanye siasa yake,mambo ya CCM atuachie  , ziko kauli ambazo Chama Cha Mapinduzi hatuna tatizo nazo zilishakwisha atuache,ni vizuri ajifakari afanye kazi ambazo zitakuwa na tija .

"Wapiga kura wengi ni vijana zaidi na wazee ni wachache ,tunasema kwa mkiki huu tunaokwenda nao miaka mitano ya kutekeleza ilani tunakwenda mara tatu zaidi ya ya miaka mitano iliyopita.Basi ni vizuri tukamaanisha watu, tumekwenda kule Pemba eneo la Mtambwe Taya ambako ndiko anatoka hajawahi kufanya kitu chochote hata kujenga mnara wa mita moja hajawahi.

"Pale Mtwambwe Taya kimejengwa kimejengwa chuo cha ufundi stadi na pale wanafunzi watasoma ,kuna shule ya bweni , ziko bweni za kutosha watoto karibu 200 watakaa pale watadundishwa ufundi wa aina mbalimbali.Na mambo hayo yote yamefanyika pale lakini huyu mzee hakufanya chochote, huyu ameshika nafasi ya uandamizi katika serikali hakufanya chochote.

"Sasa anatupotezea muda anamsema mgombea wetu , tunasema acha, hii ni mara ya mwisho,tutashulika na wewe katika namna ambayo inaweza kuleta habari nyingine, fanya kampeni za kistaarabu na sisi tumezindua kampeni juzi nzuri kabisa hatutaki kusema watu, tunasema hoja, tunajenga sababu kwa watanzania,tumepewa heshima kubwa sana katika miama mitano tumefanya kazi kubwa, kazi imefanyika kule Zanzibar."

Awali Polepole amesema kama mnavyofahamu leo agosto 31,2020 Kamati Kuu ya HAlmashauri kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti  John Magufuli imeketi jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa mchakato wa uchaguzi mkuu uliopo mbele yetu.

Amesema kwamba Kamati Kuu leo imefanya kazi moja kubwa ya kufanya uteuzi wa mwisho ndani ya Chama."Wanachama wa CCM wanaomba dhamana ya kugombea  kwa nafasi ya ujumbe wa baraza la wawakilishi kule Zanzibar.Kwa nafasi ya Baraza wa wawakilishi kule Zanzibar.

"Kamati Kuu chini ya Rais Magufuli imejadili,imetafakari na hamatimaye imefanya uteuzi wa wana CCM, watu hodari,watu mabingwa kwa maana ya uongozi, watu ambao ni kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar na mustakali wake wa sasa na baadae uko katika mikono salama.

"Uamuzi wa Kamati Kuu siku ya leo umezingatia uwakilishi wa kimakundi kwa maana makundi rika.Tunaangalia mazingira ya Zanzibar,maisha ya leo kwa kutizama uchumi wa Zanzibar  na hivyo msingi wa kuangalia watu wanaoweza kuwa na mawazo mazuri yenye kujenga,"amesema.

Ameongeza kwamba Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hasa katika chombo hiki cha dola na wawakilishi Zanzibar linapata wawakilishi ambao wanasadifu maoni ya Cha Cha Mapinduzi ,maono ya Serikali ya Jahamhuri ya Muungano wa Tanzania,maono ya mgombea wa chama cha mapinduzi kul zanzibar ndugu yetu dk.husein mwinyi.

"Tumeshajifafanua kwamba suala la maendeleo kule Zanzibar sio la mjadala lakini mwendo kasi wa kuyapaleka maendeleo hayo kwa watu wetu kule Zanzibar halina mjadala,tumefanya utafiti mkubwa , na tumejiridhisha watanzania wazanzibar wanataka ule mziki wa ndugu Magufuli katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Basi  mziki ule uwakisiwe kule Zanzibar kwa kupitia mtu mmoja,mtaratibu,mpole mnyenyekevu,mtu wa watu, mwenye nidhamu ya hali ya juu ambaye amehudumu katika dhamana ya uongozi kama kiongozi mwandamizi ,katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ,ndugu yetu Hussein Mwinyi anaweza kutuvusha, kuwafikisha mapema zaidi wazanzibar kule tunakotaka kufika kama Zanzibar na sehemu ya Jamhuri ya Muungano waTanzania,"amesema.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad