HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, August 1, 2020

BENKI YA MAENDELEO TIB YASHIRIKI NANE NANE 2020

Benki ya Maendeleo TIB inashiriki Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.


Benki ya Maendeleo ya TIB inashiriki maonesho hayo ili kutoa elimu kwa umma, kutangaza huduma inayozitoa pamoja na kuvutia wateja wapya kwa ajili ya uwekezaji katika miradi ya kimkakati nchini.


Pia, benki inatumia fursa hiyo kutoa ushuhuda wa miradi ya kimikakati iliyokopeshwa kwa wateja wake waliotapakaa nchi nzima.

Mkurugenzi wa Mipango, Mikakati na Mahusiano ya Kitaasisi wa TIB, Bw. Patrick Mongella (kushoto) akizungumza na mmoja wa wateja wa Benki hiyo kutoka Kampuni ya Mwasonge Farms, Bw. Walter Nyoni (kulia).

Baadhi ya wateja wa Benki ya Maendeleo TIB wanaoshiriki Maonesho ya Nane Nane wakionesha bidhaa wanazozizalisha.

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo TIB wakiwa tayari kuwahudumia wateja na wananchi wanaotembelea Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad