HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 5, 2020

BALOZI WA TANZANIA NCHINI UBELGIJI NA MWAKILISHI KATIKA UMOJA WA ULAYA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO



Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji na Mwakilishi katika Umoja wa Ulaya, Mhe. Jestas Abuok Nyamanga akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya, Mhe. Ursula von der Leyen katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Makao Makuu ya Umoja huo jijini Brussels, Ubelgiji tarehe 30 Julai 2020.

Wakizungumza baada ya kukamilika kwa makabidhiano hayo viongozi hao waliazimia kudumisha na kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano mzuri uliodumu kwa zaidi ya miaka 50 baina ya Serikali ya Tanzania na Umoja wa Ulaya.

Kadhalika, Mhe. Nyamanga alieleza Tanzania na Umoja wa Ulaya zimekuwa na ushirikiano wenye manufaa kwa pande zote mbili hususan katika eneo la ubia wa maendeleo kwenye sekta za kilimo, miundombinu, elimu, nishati, afya na mazingira. Hivyo, ushirikiano huo pia umehamasisha uwekezaji, biashara na kutembeleana baina ya watu wa pande zote na kuzidi kuongeza fursa kwa wananchi wake.

Tanzania na Umoja wa Ulaya pia zinashirikiana katika mikakati mbalimbali ya kutafuta na kudumisha amani, usalama na utulivu katika ukanda wa nchi za Maziwa Makuu, barani Afrika na duniani kwa ujumla.


Balozi Nyamanga akitoa maelezo mafupi kwa Mhe. Ursula von der Leyen kabla ya kuwasilisha rasmi Hati za Utambulisho.


Picha ya pamoja baada ya kukamilika kwa zoezi la kuwasilisha Hati za Utambulisho.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad