WATAFUNAJI
watakao bainika kufuja fedha za walio katika mpango wa TASAF kipindi
cha pili cha Awamu ya Tatu unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
TASAF wameonywa kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Onyo
hilo limetolewa na Mjumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi wa Mfuko wa
Maendeleo ya Jamii- TASAF, (National Steering Committee ) Eng. Rogatus
Mativila, wakati wa kufuatilia zoezi la Uhakiki lililoanza leo kwenye
Kata sita (6) Manispaa ya Morogoro.
Akizungumza
na Waandishi wa habari, Matavila, amesema kuwa kumekuwepo na Walenga
hewa sio jambo jema hata kidogo jambo ambalo limekuwa likitolewa
malalamiko sana.
“Uwepo
wa kaya hewa katika maeneo ya utekelezaji aibu sana kwa viongozi wa
mikoa, wilaya na Halmashauri.Serikali haitakuwa na huruma kwa mtu
yeyote. Kufanikiwa ama kutofanikiwa kwenye maeneo yenu itakuwa mojawapo
ya vipimo nnitakavyotumia kujua kama mastahili kuendelea na nafasi
mlizonazo au la. Siwatishi lakini huo ndio ukweli’’ Amesema Mativila.
Amesema
katika kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa, walengwa wa mpango wa
kunusuru kaya maskini watahakikiwa kwa kuondolewa au kuingizwa katika
mpango kwa kufuata vigezo vilivyowekwa a serikali.
Mativila,
amesema kuwa Uwajibikaji na uadilifu kwa wataalamu ni muhimu katika
kusimamia zoezi la uhakiki wa Walengwa wa Mpango wa TASAF ambao
utasaidia kupata Takwimu sahihi za wanufaika Halisi ndani ya Manispaa
ya Morogoro.
Amesema
kuwa, Mkazo mkubwa katika Kipindi cha Pili utawekwa katika kuwezesha
Kaya zitakazoandikishwa kwenye Mpango kufanya kazi ili kuongeza kipato
na kuhakikisha kwamba huduma za jamii zinaongezwa na kuboreshwa na
kuendeleza rasilimali watoto hususani katika upatikanaji wa elimu na
afya.
Aidha,
amesema Pamoja na hayo tathimini ya serikali ya utekelezaji wa TASAF
kipindi cha kwanza awamu ya tatu inaonyesha umaskini nchini umepunngua
kwa asilimia 10 kwa mahitaji ya msingi na umaskini uliokithiri umepungua
kwa asilimia 12 kwa kaya maskini sana nchini.
Amewasisitiza
Viongozi na Maafisa Waandikishaji Kaya kufanya kazi kwa uadilifu na
weredi wakati wa utekelezaji wa Zoezi hili kama maagizo yaliivyotolewa
na Mh Rais katika hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Kipindi cha Pili
kuhusu uwepo wa kaya hewa.
“
Uwepo wa kaya hewa katika maeneo ya utekelezaji ni aibu sana kwa
viongozi wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri. Nitoe wito kwa wahusika wote
kusimamia vizuri mradi huu. Serikali haitakuwa na huruma kwa mtu yeyote.
Kufanikiwa ama kutofanikiwa kwenye maeneo yenu itakuwa mojawapo ya
vipimo nitakavyotumia kujua kama mnastahili kuendelea na nafasi
mlizonazo au la. Siwatishi lakini huo ndio ukweli.” Amesema Mativila
Hata
hivyo amewakumbusha wananchi wote kuchukua tahadhari ya ugonjwa hatari
wa COVID-19 ili kuepuka Mikusanyiko isiyoyalazima, kuvaa barakoa,
kuepuka kushikana mikono na kunawa mikono kwa sabuni kwa kutumia maji
safi yanayotiririka pamoja na kutumia vitakasa mikono.
No comments:
Post a Comment