Wakazi
wa Mtaa wa King'azi "A" na "B" wameishukuru Serikali kwa kupata huduma
ya Maji kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam
(DAWASA), wakazi hao wamesema kulikuwa na changamoto kubwa ya
upatikanaji wa Maji katika Mitaa hiyo kabla ya ujio wa Mradi huo wa Maji
uliopo chini ya Halmashauri ya Ubungo jijini Dar es Salaam.
Wakizungumza walipotembelewa na Maafisa wa DAWASA kutokan Kitengo cha kinachosimamia Miradi ya Maji pembezoni mwa Jiji (Offgrid) wameishukuru Serikali ya Tanzania chini ya Rais wake, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kwa utendaji kazi wake sambamba na Viongozi wake wa chini.
"Tunamshukuru sana Mhe. Rais Magufuli, kwa DAWASA kufanikisha huduma hii ya Maji, tulikuwa tunanunua Maji Ndoo kubwa Moja kwa Shilingi 500 na tukiagiza Maji kwa Magari tunakaa wiki nzima baadae tunaletewa Maji kwa dumu la Lita 1000, tunalipa Shilingi 15000. Kwa kweli tunawashukuru sana DAWASA kwa kuleta huduma hii ya Maji hii ni moja ya Kututua Ndoo akina Mama", amesema Halima Sheshe, Mkazi wa King'azi B.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maji King'azi B, John Joseph Lumatu ameishukuru Serikali kupitia DAWASA kufikisha huduma hiyo karibu na Wananchi wake, pia ameomba kwa DAWASA kuangalia sehemu nyingine kuendelea kutatua changamoto hizo za upatikanaji wa Maji.
"Hatukutegemea kama tunaweza kupata Maji kama hivi, nawashukuru viongozi wote, DAWASA kufanikisha kupata huduma ya Maji katika Mtaa wa King'azi, changamoto kubwa ilikuwa Kisima kilikuwa kinasimamiwa na Kamati ya Maji kule Juu baada ya ujio wa Mkuu wa Wilaya kuvunja Kamati hiyo, hivyo kukabidhiwa DAWASA hilo tunashukuru", amesema Lumatu.
Kwa upande wake, Afisa wa DAWASA, Kitengo cha kinachosimamia Miradi ya Maji pembezoni mwa Jiji (Offgrid), Mark Stanley amesema Mradi wa Mtaa wa King'azi A na B upo chini ya Halamashauri ya Ubungo hivyo wamefanya maboresho ya mradi kuongeza vituo cha kuchotea maji nane wakati vituo vinne vipo King'azi B na vitatu mtaa wa King;azi A, Stanley amesema wataendelea kuboresha mradi huo ili lengo na azma ya Serikali kutua Mama Ndoo Kichwani itimie.
Wakizungumza walipotembelewa na Maafisa wa DAWASA kutokan Kitengo cha kinachosimamia Miradi ya Maji pembezoni mwa Jiji (Offgrid) wameishukuru Serikali ya Tanzania chini ya Rais wake, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kwa utendaji kazi wake sambamba na Viongozi wake wa chini.
"Tunamshukuru sana Mhe. Rais Magufuli, kwa DAWASA kufanikisha huduma hii ya Maji, tulikuwa tunanunua Maji Ndoo kubwa Moja kwa Shilingi 500 na tukiagiza Maji kwa Magari tunakaa wiki nzima baadae tunaletewa Maji kwa dumu la Lita 1000, tunalipa Shilingi 15000. Kwa kweli tunawashukuru sana DAWASA kwa kuleta huduma hii ya Maji hii ni moja ya Kututua Ndoo akina Mama", amesema Halima Sheshe, Mkazi wa King'azi B.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maji King'azi B, John Joseph Lumatu ameishukuru Serikali kupitia DAWASA kufikisha huduma hiyo karibu na Wananchi wake, pia ameomba kwa DAWASA kuangalia sehemu nyingine kuendelea kutatua changamoto hizo za upatikanaji wa Maji.
"Hatukutegemea kama tunaweza kupata Maji kama hivi, nawashukuru viongozi wote, DAWASA kufanikisha kupata huduma ya Maji katika Mtaa wa King'azi, changamoto kubwa ilikuwa Kisima kilikuwa kinasimamiwa na Kamati ya Maji kule Juu baada ya ujio wa Mkuu wa Wilaya kuvunja Kamati hiyo, hivyo kukabidhiwa DAWASA hilo tunashukuru", amesema Lumatu.
Kwa upande wake, Afisa wa DAWASA, Kitengo cha kinachosimamia Miradi ya Maji pembezoni mwa Jiji (Offgrid), Mark Stanley amesema Mradi wa Mtaa wa King'azi A na B upo chini ya Halamashauri ya Ubungo hivyo wamefanya maboresho ya mradi kuongeza vituo cha kuchotea maji nane wakati vituo vinne vipo King'azi B na vitatu mtaa wa King;azi A, Stanley amesema wataendelea kuboresha mradi huo ili lengo na azma ya Serikali kutua Mama Ndoo Kichwani itimie.
Pia amesema kuna mchakato unafanyika ili kuhamisha mradi huo
chini ya Halamashauri ya Ubungo na kupelekwa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) ili kongeza ufanisi kwenye utendaji kazi wa Mamlaka hiyo.
chini ya Halamashauri ya Ubungo na kupelekwa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) ili kongeza ufanisi kwenye utendaji kazi wa Mamlaka hiyo.
Mjumbe
wa Serikali ya mtaa King'azi "B", Halima Twalib akimwagiwa maji na
wakazi wa mtaa huo kwa kuonesha furaha mara baada ya maji ya Mamlaka ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam, (DAWASA) kutoka kwa mara
ya kwanza ikiwa ni jitihada za mjumbe huyo kufanikiwa upatikanaji wa
maji katika Mtaa wa King'azi "B" kata ya Kwembe Manispaa ya Ubungo
jijini Dar es Salaam
Mwanyekiti
wa Serikali ya mtaa King'azi "A", Juma said Msumali akitolea ufafanuzi
wa mradi wa maji ulioko chini ya Manispaa ya Ubungo ambapo uko kwenye
mchakato wa kutolewa kwenye manispaa na kupewa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam, (DAWASA) kwa ajili ya usambazaji katika mtaa wa Kwembe hasa kwenye mtaa wa King'azi "A" na "B".
Afisa
wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam, (DAWASA)
kutoka kwenye kitengo kinachosimamia miradi ya maji pembezoni mwa jiji (
Offgrid) Mark Stanley akitoa ufafanuzi wa mradi wa maji wa King'azi "A"
na "B" unaotakiwa kutoka Manispaa ya Ubungo na kwenda DAWASA wakati wa
ziara ya kuhakikisha maji yanatoka katika vituo vilivyowekwa na DAWASA.
Mwenyekiti
wa Kamati ya maji mtaa wa King'azi "B", John Joseph Lumatu(wa pili
kushoto) akitoa maelezo kwa maofisa wa DAWASA kuhusu namna
walivyojipanga kama kamati ya maji ya mtaa ili kuhakikisha wananchi wa
mtaa huo wanapata maji kwa wakati ili kuondoa hadha ya upatikanaji wa
maji iliyokuwa inawakabili.
Afisa
wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam, (DAWASA)
kutoka kwenye kitengo kinachosimamia miradi ya maji pembezoni mwa jiji (
Offgrid) Mark Stanley akitoa ufafanuzi kuhusu namna DAWASA
ilivyojipanga katika usambazaji wa maji katika mitaa ya King'azi "A" na "B" ili kumtua mama ndoo kichwani.
Afisa
wa Habari kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam, (DAWASA), David Nkulila akishuhudia wananchi wanavyochota maji
ya DAWASA katika mtaa wa King'azi "B" ikiwa ni majaribio ya usambazaji wa maji katika mtaa huo na mitaa mingine katika kata ya Kwembe Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam.
Maofisa
kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam,
(DAWASA) wakishuhudia utokaji wa maji kwa mara ya kwanza katika mtaa
wa King'azi B kwenye mradi wa maji wa DAWASA uliokuwa katika Manispaa
ya Ubungo wakati wa majaribio wa usambazaji wa maji katika kata ya ya
Kwembe Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam.
Afisa
wa Dawasa kutoka kwenye kitengo kinachosimamia miradi ya maji pembezoni
mwa jiji ( Offgrid) Mark Stanley akitolea ufafanuzi moja ya kisima cha
maji kinachosambaza maji katika mtaa wa King'azi "B" kata ya ya Kwembe Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment