HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 30, 2020

KOKA ATOA MIZINGA YA NYUKI KWA JUMUIYA YA WAZAZI

KOKA AIPATIA JUMUIYA YA WAZAZI KIBAHA MIZINGA YA NYUKI 
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Mjini, Slyvestry Koka, amekabidhi Mizinga kumi ya Nyuki Yenye Thamani ya Shilingi Milioni 1.5 kwa Umoja wa Wazazi(CCM) Kibaha Mjini kwa Ajili ya Mradi wa Ufugaji wa Nyuki.

Akizungumza Wakati wa Makabidhiano Hayo, katika Ofisi za CCM Kibaha Mjini, Jana, Mbunge Koka Aliipongeza Jumuiya Hiyo kwa Kupata Mwenyekiti Mwenye Maono Makubwa ya Kuiendeleza Jumuiya Hiyo kwa Kuitafutia Miradi Mbalimbali.

"Niwapongeze Jumuiya ya Wazazi Kibaha Mjini kwa Kupata Mwenyekiti Shunda Ambaye Anajitambua,Mbunifu na Mckarikaji katika Kutaka Kuacha Alama kwa Muda Aliopo Madarakani katika Utawala Wake;

Aidha Mbunge Koka, Alisema kwa Hamasa ya Maendeleo ya Jumuiya ya Wazazi Imempelekea Yeye Kama Mwakilishi katika Jimbo Hilo la Kibaha Mjini Kutoa Mizinga 10 Kwa Ajili ya Kuchagiza na Kutunisha Mradi wa Ufugaji wa Nyuki Ambao Baada ya Uvunaji wa Asali Utaipatia Jumuiya Hiyo Kipato.

Akizungumza Baada ya Kupokea Mizinga Hiyo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi Tanzania Jumuiya ya CCM, Edwin Shunda, Alimshukuru Mbunge Koka kwa Kuipatia Jumuiya Hiyo Mizinga 10 na Kusema Awali Walikuwa na Mizinga 30 kwa Kuongezewa Mizinga 10 Sasa Mizinga imefika 40.

"Kwa Niaba ya Jumuiya ya Wazazi Kibaha Mjini Tunamshukuru Mbunge Koka kwa Kutupatia Mizinga 10 ya Nyuki Tayari Tuna Mizinga 30 Ambayo Tumeshatundika Kwenye Shamba Letu na Hii 10 Jumla 40" Alisema Mwenyekiti Shunda.

Pia Mwenyekiti Shunda Alitumia Nafasi Hiyo Kuwashukuru Meneja wa Kanda wa Wakala wa Misitu Tanzania na Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti wa Miti Dawa Kutoka Muhimbili kwa Kuipatia Jumuiya Hiyo ya Wazazi Shamba Ekari 5 na Maji kwa Ajili ya Ufugaji wa Mradi wa Nyuki Utakaozalisha Asali Baada ya Uvunaji na Kuiletea Fedha Jumuiya Hiyo.



1 comment:

  1. Hongera kwake mh koka kwa kuwajali wananchi wake wa mkoa wa pwani.pia aaa hiyo ni fursa msiache kuwa na mwendelezo.tuyatunze mazingira

    ReplyDelete

Post Bottom Ad