HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, October 21, 2019

Waziri Mkuu azindua Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Pwani

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akitoa hotuba wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akizundua Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Mh. Angellah Kairuki (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto).
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akionyesha nakala za Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Mh. Angellah Kairuki (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto).
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akimkabidhi nakala Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo mara baada ya kuzindua Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Mh. Angellah Kairuki akizungumza wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akitoa salamu za ukaribisho kwa wageni waalikwa na wananchi (hawapo pichani) wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akizungumza wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Amon Manyama akitoa salamu za Umoja wa Mataifa wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Mwakilishi wa timu ya ESRF iliyoshiriki kuandaa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani, Prof. Samuel Wangwe akiwasilisha mada wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akibadilishana mawazo na Mkuu wa Idara ya Maarifa na Ubunifu ya Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Magreth Nzuki walipokuwa wakisubiri kuwasili kwa mgeni wa heshima kwenye Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Wawakilishi wa timu iliyoshiriki kuandaa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani, Mkuu wa Idara ya Maarifa na Ubunifu ya Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Magreth Nzuki (katikati) na Prof. Samuel Wangwe (kushoto)wakibadilishana mawazo walipokuwa wakisubiri kuwasili kwa mgeni wa heshima kwenye Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mh. Jokate Mwegelo wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Baadhi ya viongozi wa taasisi za serikali na sekta binafsi walioshiriki Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa katika picha ya pamoja na timu ya ESRF wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakuu wa wilaya wa mkoa wa Pwani wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa katika picha ya pamoja na wawekezaji wakati wa Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Pwani lilioenda sambamba na uzinduzi wa Mwongozo na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Pwani uliondaliwa na ESRF chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Pwani mjini Kibaha.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa (MB) amezindua Mwongozo wa  Uwekezaji wa Mkoa wa Pwani katika Ukumbi wa Mkutano wa Ofisi ya Mkoa wa Pwani sambamba na kufungua rasmi Kongamano la Uwekezaji katika Mkoa Pwani mwishoni mwa wiki.
Katika Uzinduzi Mwongozo huo, Waziri Mkuu alichukua fursa hiyo pia kuitaka mikoa ambayo bado haijatekeleza agizo lake la kuandaa makongamano ya uwekezaji ihakikishe inafanya hivyo mara moja. 
 “Nitumie fursa hii kuwapongeza viongozi wa mkoa wa Pwani kwa kutekeleza agizo nililolitoa Juni 18, 2018 wakati wa Kongamano la tatu la uwezeshaji wananchi kiuchumi la kuhakikisha mikoa yote inaandaa Kongamano la Uwekezaji na inakuwa na Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa. Mikoa ambayo haijatekeleza agizo hilo, ifanye hivyo mara moja,” amesema.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri wahakikishe wanasimamia miundombinu inayoelekea kwenye viwanda vilivyopo kwenye maeneo yao.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa Kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Angella Kairuki alisema kwamba Serikali imeanza kutekeleza mapendekezo ya mpango wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini (Blueprint for Regulatory Reforms for Improving the Business Environment) kwa kuondoa tozo zaidi ya 163 zilizokuwa zikilalamikiwa na wawekezaji.
“Pia tumetenganisha majukumu ya TBS ya TFDA ambayo sasa ni TMDA. TBS itashughulika na vyakula na TMDA itashughulika na dawa na vifaatiba. Vilevile, tumeondoa ada za usajili sehemu za kazi ambazo zamani ilikuwa ni sh. 28,000 na sasa hivi zinatolewa bure,” alisema.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mheshimiwa Mhandisi Evarist Ndikilo aliwataka watu wote wanaotaka kuwekeza nchini waufikirie kwanza mkoa wa Pwani kwa sasabu uko kimkakati na una fursa nyingi ikiwemo hali nzuri ya usalama na kwa maana hiyo mitaji yao italindwa.
“Mkoa wetu uko kwenye eneo la kimkakati la kuwezesha biashara kwa kuwa uko karibu na bandari ya Dar es Salaam na uwanja wa ndege; uko karibu na soko kubwa ambalo ni Dar es Salaam; unapitiwa na reli zote kwenda mikoani na nchi jirani; unapitiwa na barabara kuu itokayo Dar es Salaam na pia una bandari kavu ya Kwala.”
Mbali ya hivyo, Mkuu huyo wa Mkoa alisema faida nyingine ambayo mkoa huo unayo ni uwepo wa miundombinu ya maji, umeme na nishati ya gesi asilia ambayo imeanza kutumiwa na baadhi ya viwanda kama Goodwill na Lodhia Steel.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Dkt. Tausi Kida alisema, Taasisi yake ikishirikiana na Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) imekuwa wa ikiandaa Miongozo ya Uwekezaji katika Mikoa kwa lengo la kuchambua na kuainisha fursa za uwekezaji zilizopo katika mikoa husika ili kuwavutia wawekezaji.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji ESRF Dkt. Tausi Kida wakati akizungumzia mchango wa Taasisi yake kwenye uandaaji wa Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Pwani, kazi ambayo imewezesha kuwapo wa Kongamano la Uwekezaji katika Mkoa huo.
Dkt. Kida alisema kwamba tayari Taasisi hiyo imesaidia Mikoa 17 kuandaa Miongozo ya Uwekezaji ambapo mikoa 12 imekamilisha na Mikoa 5 iko katika hatua mbalimbali.
“Hadi sasa tumekwishaisadia mikoa 17 kuandaa Miongozo ya Uwekezaji na kwa sasa mikoa 12 imeshakamilisha na mikoa mitano iko kwenye hatua mbalimbali,” alisema.
Akizungumzia Mkoa wa Pwani, Dkt Kida alisema Mkoa Pwani una fursa nyingi katika Sekta za; Viwanda, Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Utalii, Madini, Miundombinu na Huduma za jamii na  kusema maelezo ya kina yapo katika Mwongozo ambao Waziri Mkuu aliouzindua.
Kwa mujibu wa Dkt. Kida, timu ya ESRF iliyoshiriki kuandaa Mwongozo huo ilijumuisha Prof. Samuel Wangwe, Bi. Margareth Nzuki, Dk Hussein Nassoro, Bw. Mussa Mayala Martine, na Bw. James Kasindi wakishirikiana na wataalam wa Mkoa wa Pwani.
Mwongozo huo ulielezwa kwa kina katika kongamano, katika mada iliyowasilishwa na Prof Samuel Wangwe.
Akitoa taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Abdulmajid Nsekela ambao ni wadhamini wakuu wa kongamano hilo, Ofisa Mkuu wa Biashara, Benki ya CRDB, Dk Joseph Witts alisema benki hiyo imeendelea kugusa sekta zote za uchumi na hivyo kuongeza tija kwenye mnyororo mzima wa uzalishaji. Alisema huduma zao zimelenga kuongeza tija na ufanisi katika sekta ya viwanda nchini ikiwemo utoaji wa mikopo ya biashara kwa ajili ya kuongeza mikopo ya uendeshaji (working capital loans) na mikopo ya uwekezaji (investment loans).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad