NA VICTOR MASANGU, PWANI
Naibu Waziri wa elimu sayansi na teknolojia Williamu Ole Nasha
amechukizwa kuona vitendo vya baaadhi ya wazazi wa jamii ya wafugaji
kutothamini suala la elimu na kuamua kuwaozesha watoto wao mapema na
kuwatumikisha katika kazi za kuchunga mifugo ambapo amekemea na
kulaani vikali vitendo hivyo na kuwataka kuhakikisha wanawapeleka
watoto wao shule ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano
katika sekta ya elimu ikiwemo utoaji wa elimu bure..
Ole Nasha ametoa kauli hiyo wakati wa halfa ya uwekaji wa jiwe la
msingi katika mradi wa ujenzi wa ofisi ya serikalI ya kijiji cha
Kigoda kilichopo katika kata ya Gwata Wilaya ya Kibaha sambamba na
kutembelea eneo maalumu ambalo limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa
shule ya sekondari ya kata ambayo itaweza kuwa mkombozi mkubwa kwa
wanafunzi ambao wamekuwa wakitembea umbari wa kilometa nane kwenda
kutafuta huduma ya elimu katika maeneo mengine.
Aliongeza kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano ni kuboresha sekta
ya elimu katika ngazi zote hivyo kitu kikubwa ni kuhakikisha watoto
wanapatiwa malezi bora ikiwemo kuwapeleka shule lengo ikiwa ni
kuwapatia ujuzi na mahalifa ambao utaweza kuliletea taifa maendeleo.
“Nampongeza sana Mbunge wa jimnbo la Kibaha Vijijini kwani amekuwa ni
mtu mwenye kunisumbua sana lakini lengo lake kubwa ni kuwaletea
maenedeleo wananchi wake, kwa hiyo kikubwa zaidi tumuunge mkono katika
kuleta mabadiliko na hili tabia ya kuwaozesha watoto wenu kwa kweli
mimi nataka muiache kabisa na kuwachungisha ng’ombe,”alisema.
Mmoja wa wazazi wa jamii ya wafugaji akizungumza kwa niaba ya
wenzake aliahidi kulitekeleza na kulivalia njuga agizo ambalo
limetolewa na Naibu Waziri na kwamba wataweka mipango madhubuti ya
kuwapatia watoto wao haki zao za msingi ikiwemo kuwapeleka shule
pamoja na kuachana na tabia ya kuwatumiksiha kwa kipindi kirefu katika
kuchunga
Naye Mbgunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Hamoud Jumaa katika kuunga
juhudi za Rais wa awamu ya tano Dk. John Pombe ,Magufuli katika sekta
ya elimu ameamua kutoa eneo la hekari kumi pamoja na kuahidi ujenzi
wa madarasa mawili kwa lengo la kuanzisha mradi wa ujenzi wa shule ya
kata ya Gwata ambayo itapunguza kwa kiasi kikubwa adha na kero kwa
wanafunzi ambao wamekuwa wakitumia muda wao mwingi wakiwa njiani
kuelekea shuleni.
“Kwanza kabisa napenda kumpongeza Naibu waziri wa elimu kwa kuja
kufanya ziara katika kijiji hiki na mimi napenda kumuahidi kuwa
maelekezo yake yote ya kuongeza hekari zingine mimi nipo tayari kwa
hiyo mimi ninatongeza hekari zingine tano kwa hiyo jumla zitakuwa kumi
hii yote ni kuhakikisha tunaunga mkono juhudin za serikali ya awamu ya
tano katika kuboresha elimu,”alisema Jumaa.
Aidha Jumaa katika hatua nyingine amesema lengo lake kubwa ni
kuhakikisha kwamba analeta mabadiliko chanya ya kimaendeleo katika
Nyanja mbali mbali na kwamba atashirikiana bega kwa bega na wananchi
pamoja na serikali kwa jili ya kukamilisha mradi wa ujenzi wa shule
hiyo ya kata ya Gwata ambayo itakuwa ni msaada mkubwa katika
kuwaondolewa wanafunzi changamoto ya kutembea umbari mrefu.
Pia aliwaasa wazazi na walezi wa jamii ya wafugaji kumuunga mkono Rais
wa awamu ya tano Dr.John Pombe Magufuli katika kuhakikisha kwamba
watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanapelekwa mara moja ili
kuwapatia haki yao ya msingi pamoja na kuwataka kuachana na tabia ya
kuwakatisha masomo bila sababu zozote za msingi.
KUMEKUWEPO na wimbi la baadhi ya jamii ya wafugaji katika Wilaya ya
Kibaha Mkoani Pwani kuamua kuwakatisha watoto wao masomo na
kuwatumikisha katika kazi mbali mbali ikiwemo kuwapeleka maporini kwa
ajili ya kuchunga ng’ombe na mbuzi pamoja na wengine kuwaozesha kitu
ambacho kinawanyima kupata haki zao za msingi ikiwemo suala la elimu.
Mbunge wa Jiambo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa kushoto akikabidhiwa zawadi ya fimbo na mmoja wa viongozi wa jamii ya wafugaji alipowasili katika kijiji cha Kigoda, kulia kwake ni Naibu waziri wa elimu sayansi na teknolojia William Ole Nasha baada ya kuwasili katika eneo hilo kwa lengo la kuweka jiwe la msingi katika ofisi ya kijiji hicho pamoja na kutembelea eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya kata (PICHA NA VICTOR MASANGU)
Naibu waziri wa elimu sayansi na teknolojia wa kati kati akipiga makofi katika halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi katika ofisi ya kijiji cha kigoda kilichopo kata ya Gwata katika halmashauri ya Kibaha vijini kushoto kwake ni Mbunge wa Kibaha Vijijini Haoumd Jumaa, na viongozi wengine wa kijiji hicho.
Naibu waziri wa elimu William Ole Nasha kushoto akiwa katika halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi pamoja na kutembelea eneo la ambalo limetengwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa shule mpya ya kata ya Gwata.kulia kwake ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Haoumd Jumaa.
Mbungewa Jimbo la Kibaha vijijini Haoumd Jumaa akizungumza
na baadhi ya wananchi wa kata ya Gwata hawapo pichani wakati wa
sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi kwa ajaili
ya ofisi ya kijiji cha kigoga pamoja na kujoinenea eneo ambalo
limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya kata(PICHA NA VICTOR
MASANGU)
No comments:
Post a Comment