BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya
Kinondoni limemchagua Mhe.George Manyama kutoka
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Naibu Meya wa
Halmashauri hiyo kwa awamu ya nne tangu mwaka 2016.
Uchaguzi huo umefanyika leo (jana) katika baraza
maalumu la madiwani la robo ya mwaka ambapo jumla
ya wajumbe 21 ambao ni madiwani walishiriki uchaguzi
huo. 
Akitangaza matokeo hayo, Katibu tawala wa Halmashauri
hiyo Bi Stella Msofe amesema kuwa idadi ya kura
zilizopigwa ni 21 kulingana na wajumbe wa baraza hilo
kutoka vyama vyote vyenye madiwani katika baraza hilo.
Msofe amemtangaza Mhe. Manyama kutoka CCM kuwa
mshindi wa nafasi hiyo ya Naibu Meya kwa kupata kura
13, huku mpinzani wake Mhe. Phares Lupomo kutoka
chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema akipata
kura nane.
Awali wagombea hao wawili walipata nafasi ya kunadi
sera zao kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo ikiwa ni
Toggle screen reader support.
No comments:
Post a Comment