

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (wa tatu kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Kanuni za Mwenendo za Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) pamoja na Mwenyekiti wa Umoja huo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kulia) katika Mkutano wa Umoja wa Mabenki, uliofanyika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es salaam. Kushoto ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florance Luoga na kulia ni Waziri wa Viwanja na Biashara, Innocent Bashungwa.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (wa pili kushoto) akipokea zawadi maalumu kutoka kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) na Makamu wake, Sanjay Rughani, baada ya uzinduzi rasmi wa Kanuni za Mwenendo za Umoja wa Mabenki Tanzania, uliofanyika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Viwanja na Biashara, Innocent Bashungwa na kushoto ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florance Luoga.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), Abdulmajid Nsekela, Makamu wake, Sanjay Rughani pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania, Tusekelege Mwaikasu-Jounde, wakikabidhi zawadi ya ngoma maalum kwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florance Luoga, baada ya uzinduzi rasmi wa Kanuni za Mwenendo za Umoja wa Mabenki Tanzania, uliofanyika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment