HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 29, 2019

WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ILI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

WANANCHI kote nchini hasa wanawake wameshauriwa na kutakiwa kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo ili kuweza kujiongezea kipato  binafsi na kuondokana na umaskini.

Akizungumza katika kongamano maalum la wanawake la malkia wa nguvu lililofanyika leo jijini Dar es Salaam mwenyekiti wa taasisi isiyo ya serikali ya Nafanikiwa Inspiration Reuben Ndimbo  amesema kuwa  kuna kila aina ya fursa nchini ambayo ikitumiwa vyema itaeleta matunda, hivyo watanzania wanatakiwa kuzichangamkia ili ziweze kuwanufaisha wao binafsi na taifa kwa ujumla.

Aidha ameongeza kuwa kutokana na kasi ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Joseph Magufuli kufungua ya uwekezaji katika sekta ya  viwanda  ni vyema sasa kila mwenye nafasi kuwekeza katika viwanda vidogo, vya kati na vikubwa.

Kwa upande wake muandaaji na mwenyekiti wa umoja wa  Malkia wa nguvu, Grace Mpanduka amesema kuwa wanawake  ni walengwa wakubwa katika kongamano hilo kutokana na uchakalikaji wao wa na wanaaminika katika kuchangamkia na kuzitendea kazi fursa zinazopatikana hapa nchini.

Amesema  kuwa nafasi ya uenyekiti wa SADC kwa Rais Dkt John Joseph Magufuli  ni fursa kubwa sana kwa watanzania  na hatuna budi kuongeza ubunifu katika nyanja mbalimbali ikiwemo nyanja za utalii, na ubunifu katika mambo mengine mengi. 

"Mimi nimejitolea kuwafungua na kuwaelimisha watanzania  wenzangu hasa akina mama ili wafahamu nchi za wenzetu wanavyochangamkia fursa  kama hizi pindi zinapotokea katika nchi zao, mwaka huu mmoja wa uenyekiti wa Rais Magufuli katika nchi za SADC ulete mabadiliko nchini" Amesema.

Aidha amempongeza Rais Magufuli kwa uchapakazi na ufunguaji  milango ya fursa kwa wanawake kwa kuwataka kuchapa kazi kwa kuanzisha viwanda na biashara zingine zitakazo itangaza nchi yetu katika mataifa ya nje.

Pia amewaomba wanawake kutumia nafasi ya SADC  kufungua milango kwa kwenda nje ya nchi kujifunza jinsi wenzetu wanavyochangamkia fursa kama za namna hiyo pamoja na ubunifu wanaotumia katika kufanya biashara.

Mgeni rasmi wa kongamano la Malkia wa nguvu na muigizaji wa filamu nchini Hidaya Njaidi 
akiangalia bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na wanawake katika njanja mbalimbali wakati wa kongamano hilo, leo jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti na mwandaaji wa umoja wa Malkia wa Nguvu,Grace Mpanduka (kulia) akizungumza na baadhi wa waandishi wa habari mara baada ya kufungua kongamano maalum la wanawake la malkia wa nguvu , ambapo amewashauri wanawake kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo ili kujikwamua kiuchumi, leo jijini Dar es Salaam.

 Mwenyekiti wa taasisi ya Nafanikiwa Inspiration,Reuben Ndimbo(katikati) akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano la maalum la wanawake la malkia wa nguvu ambapo amewashauri wananchi kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano katika ujenzi wa uchumi, leo jijini Dar es Salaam.
  Mgeni rasmi na muigizaji wa filamu nchini Hidaya Njaidi akiwasili katika ukumbi wa TGNP uliopo Mabibo jijini Dar es Salaam ili kuendelea na shughuli ya kongamano la Malkia wa nguvu


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad