HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 29, 2019

WAKAZI WA MLANDIZI-MBOGA KUONDOKANA NA SHIDA YA MAJI FEBRUARI 2020-MWAMUNYANGE

 Mkurgenzi wa Uzalishaji na Usambazaji DAWASA Aron Joseph akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Bodi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange  baada ya kutembelea mtambo wa Ruvu juu unaozalisha maji Lita Milioni 196 kwa siku wakati wa ziara ya bodi ya DAWASA  kuangalia na kukagua maendeleo ya miradi mbalimbali ya Mamlaka hiyo
Mkurgenzi wa Uzalishaji na Usambazaji DAWASA Aron Joseph akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Bodi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange  baada ya kutembelea mtambo wa Ruvu juu unaozalisha maji Lita Milioni 196 kwa siku wakati wa ziara ya bodi ya DAWASA  kuangalia na kukagua maendeleo ya miradi mbalimbali ya Mamlaka hiyo
Mkurgenzi wa Uzalishaji na Usambazaji DAWASA Aron Joseph  akimuoneshaMwenyekiti wa Bodi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange  pampu zitakazotumika kusukuma maji kuelekea kwenye mradi wa maji wa  Mlandizi -Chalinze Mboga wenye urefu wa Km 59 wakati wa ziara ya bodi ya DAWASA kutembelea miradi mbalimbali ya Mamlaka hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange akizungumzia mradi wa maji wa Mlandizi -Chalinze Mboga wenye urefu wa Km 59 na utakapokamilika utahudumia wananchi 120,000 na maji yatakayosafirrishwa ni lita milioni 9 kwa siku.
Mkurugenzi wa Miradi DAWASA Mhandisi Ramadhan Mtindasi akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Bodi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange baada ya kutembelea mradi wa Mlandizi-Chalinze Mboga.
 
Mafundi na Wakandarasi wakiendelea na zoezi la kuondoa mawe makubwa kwa ajili ya ulazaji wa mabomba ya maji kutoka kwenye mtambo ws Ruvu Juu kuelekea Mlandizi Chalinze Mboga.
Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

Kukamilika kwa Mradi wa Maji Mlandizi -Chalinze Mboga kutaondoa kero ya maji kwa wananchi wa Chalinze, Mlandizi na maeneo mengine ya Karibu.

Mradi huo wenye thamani ya Bilion 16, unatarajia kumalizika ifikapo Februari 2020 na utahudumia wakazi 120,000.

Akiwa katika ziara ya kutembelea mradi huo , Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na Majitaka DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange amesema kukamilika kwa mradi huu kutasaidia kuondoa kero ya muda mrefu ya maji .

Amesema, mradi huo umeanza kutekelezwa Mwezi Juni mwaka huu na unakadiriwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Februari 2020 na ukikamilika utakuwa na uwezo wa kusafirisha maji Lota Milion 9 kwa siku.

“Kuna changamoto imeweza kujitokeza, tulikua tunajadiliana na wakandarasi tumeona miamba ikiwa ni mikubwa kwenye njia ya ulazaji mabomba na wameweza kuiondoa na kuendelea na zoezi la uchimbaji na kulaza mabomba,”amesema Mwamunyange

Naye Mkurugenzi wa Miradi DAWASA Mhandisi Ramadhan Mtindasi mradi wa Mlandizi-Chalinze Mboga ni mpango wa kuondoa tatizo la maji kwenye mji mdogo wa Mboga na maeneo ya Viwanda.

“Mradi huu unachukua maji kutoka Mtambo wa Ruvu juu na tutajenga kituo kidogo cha kusukuma maji kwenye eneo la Chamakweza na Msoga na utawanufaisha wakazi wa Vigwaza, Chalinze na maeneo yote yanayopita mradi huo na tutaweka vituo kwa ajili ya kutoa huduma ya maji,”amesema Mtindasi.

DAWASA wameweka mikakati ya kufikia asilimia 95 ya wananchi kupata maji safi na salama kufikia 2020 kwa mijini na asilimia 85kwa vijijini ambapo kwa sasa miradi mbalimbali inaendelea kujengwa na mingine kuboreshwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad