HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 20, 2019

Benki ya Maendeleo TIB yawapiga msasa Wataalam 150 wa Maandiko ya Miradi ya Maendeleo

Wataalam kutoka Benki ya Maendeleo TIB imetoa darasa kuhusu maandiko ya miradi ya maendeleo yenye kukopesheka (bankable projects) kwa wataalam wa maandiko kutoka mikoa minne inayojumuisha mikoa ya Mtwara, Lindi, Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani.

Mafunzo hayo yaliongozwa na Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati, Bw. Patrick Mongella kwa kusaidiana na Meneja Uendelezaji Biashara, Bw. Joseph Chilambo na Meneja Miradi Maalum, Bw. Derick Moshi.
Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Patrick Mongella akitoa utambulisho wa Programu Maalum na Huduma za Fedha za Benki ya Maendeleo TIB.
Meneja Uendelezaji Biashara wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Joseph Chilambo akiwasilisha mada kuhusu Huduma za Fedha kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na Maandilizi yake kwa wataalam wa maandiko kutoka mikoa ya Mtwara, Lindi, Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani.
Meneja Miradi Maalum wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Derick Moshi akitoa elimu kuhusu Uchambuzi wa Miradi ya Maendeleo kwa wataalam wa maandiko kutoka mikoa ya Mtwara, Lindi, Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani.
Wataalam wa maandiko kutoka mikoa ya Mtwara, Lindi, Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani wakifuatilia kwa makini mafunzo kuhusu maandiko ya miradi yenye kukopesheka (bankable projects).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad