Naibu
 Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, 
Antony Mavunde (wa pili kushoto), akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi 
milioni nne kwa mshindi wa kwanza wa shindano la michoro ya usalama 
barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi mwaka 2019, Alphonce Philipo
 wa shule ya msingi Jenerali Musuguri, katika hafla iliyofanyika jijini 
Dodoma jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, 
waandaaji wa shindano, Dominic Dhanah

Naibu
 Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, 
Antony Mavunde,akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule
 za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa 
mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika 
katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Mkurugenzi
 Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, waandaaji wa shindano, Dominic 
Dhanah,akisoma taarifa katika utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za
 msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 
2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika
 shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Mkurugenzi
 Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, waandaaji wa shindano, Dominic 
Dhanah,akifurahia jambo na wanafunzi (hawapo pichani) wakati akisoma 
taarifa inayohusu utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi 
walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 
yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika 
shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Mratibu
 wa mafunzo ya Elimu ya usalama barabarani kutoka Amend Bi.Neema 
Swai,akiongea wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi 
walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 
yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika 
shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Mwalimu
 wa shule ya Msingi ya General Musuguri,Beatrice Chidumizi,akitoa 
pongeza kwa Puma Energy wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za
 msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 
2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika
 shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Afisa
 Elimu Msingi jiji la Dodoma,Joseph Mabeyo,akitoa shukrani kwa Kampuni 
ya Mafuta ya Puma Energy Tanzania wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi 
wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani
 kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo 
imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Naibu
 Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, 
Antony Mavunde (wa pili kulia), akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa 
Puma Energy Tanzania, waandaaji wa shindano, Dominic Dhanah, wakati wa 
kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la 
Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma 
Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni 
jijini Dodoma .

Mwalimu
 wa shule ya msingi Kaloleni Bi.Edina Kagulumbega,akizungumza wakati wa 
kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la 
Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma 
Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni 
jijini Dodoma .



Sehemu
 ya Wanafunzi kutoka shule za msingi wakifuatilia hafla ya utoaji wa 
zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro 
ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy 
Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini 
Dodoma .

Baadhi
 ya walimu wakifuatilia utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za 
msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 
2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika
 shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Wanafunzi
 wakiimba wimbo maalumu wa unaoelezea umuhimu wa kuzingatia sheria za 
usalama barabarani wakati wa utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za 
msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 
2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika
 shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Mmoja
 wa wanafunzi waliopata elimu ya mafunzo ya usalama barabarani akionesha
 mfano wa mwanafunzi aliyepata ajali kwa kutozingatia sheria za usalama 
barabarani wakati wa utoaji zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi 
walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 
yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika 
shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Wakiangalia
 michoro ya usalama barabarani iliyochorwa na wanafunzi kutoka shule 
tano za msingi katika jiji la Dodoma kabla ya kumtangaza mshindi wa 
shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa 
na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi 
Kaloleni jijini Dodoma .

Naibu
 Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, 
Antony Mavunde,akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa shindano la 
michoro ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi mwaka 
2019, hafla ambayo imefanyika jijini Dodoma.
......................
*Ni katika mkakati wake wa kukomesha ajali nchini, wanafunzi Dodoma wanufaika
*Naibu Waziri Mavunde awapongeza, asema ni kampuni ya mfano...atoa maombi maalum
Na Said Mwishehe,Michuzi TV -Dodoma
KAMPUNI
 ya Puma Energy Tanzania imesema itaendelea kutoa elimu ya mafunzo ya 
usalama barabarani kwa shule za msingi mbalimbali nchini ikiwa ni 
mkakati wake wa kupunguza ajali nchini.
Pamoja
 na ahadi hiyo kampuni hiyo imetoa mafunzo ya usalama barabarani kwa 
wanafunzi zaidi ya 4500 katika shule tano za msingi katika Jiji la 
Dodoma kwa mwaka huu wa 2019 huku ikiahidi kuendelea kutoa elimu hiyo na
 kufanya kazi kwa karibu na Serikali ili kuhakikisha elimu hiyo 
inawafikia wanafunzi wengi zaidi ambao watakuwa mabalozi kwa wengine.
Akizungumza
 leo Julai 25 jijini Dodoma mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri 
Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Vijana Athony Mavunde, Mkurugenzi Mtendaji 
wa Puma Energy Tanzania Dominic Dhanah amesema programu hiyo ya mwezi 
mmoja kwa Dodoma ilihusisha mafunzo ya usalama barabarani kwa walimu 15 
na wanafunzi 4500, katika shule tano.
Amefafanua
 kulikuwa na shindano la uchoraji wa michoro inayo hamsisha usalama 
barabarani ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni iliyozinduliwa rasmi
 mwaka 2013 ambapo zaidi ya shule 80 zimefikiwa huku wanafunzi 100,000 
wakiwa wamepatiwa mafunzo katika mikoa ya Dar-es-salaam, Geita, Ruvuma 
na Dodoma.
“Puma
 Energy Tanzania imeamua kuja jijini Dodoma kwa sababu ya ukuaji wa 
haraka wa jiji hili ambapo shughuli za kijamii na ongezeko la watu na 
magari ambayo yanahatarisha usalama wa watoto wanapokwenda shuleni na 
kurudi nyumbani,",amesema Dhanah na kuongeza “Hadi sasa tumeweza 
kufundisha wanafunzi zaidi ya 4500 wa shule tano za msingi zilizopo jiji
 la Dodoma".
Dhahana
 amesema mafunzo hayo ya usalama barabarani na uchoraji alama za 
barabarani ni kipaumbele kwa lengo la kuwapa uelewa watoto hususani wa 
shule za msingi juu ya namna bora ya matumizi ya barabara.Alibainisha
 lengo ni kuwafanya watoto kuwa na uelewa wa matumizi ya barabara ili 
kuongeza uelewa kuhusu dhima nzima ya usalama barabarani kwa Watanzania.
“Lengo
 letu kama kampuni ni kuongeza wigo ili kufikia shule nyingi zaidi nchi 
nzima. Puma Energy Tanzania itaendelea kuwekeza katika kampeni ya 
usalama barabarani ikishirikiana na serikali kupitia jeshi la Polisi ili
 kuokoa maisha ya watanzania,” amebainisha.Akieleza
 zaidi amesema unzo hayo yametolewa na Kampuni ya Mafuta ya Puma 
Tanzania kupitia Shirika lisilo la kiserikali la Amend ambapo elimu hiyo
 pia imetolewa kwa walimu 15 wa shule hizo.
Awa
 upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi ,Ajira 
na Vijana Anthony Mavunde amesema Puma Energy Tanzania ni kampuni 
iliyoamua kutoa elimu ya usalama barabara nchini huku akitoa ombi kwa 
kampuni hiyo kufundisha walimu hizo ili wakifundisha masomo ya kawaida 
wawe pia wanataka na elimu ya usalama.
Amesema
 kwa kufanya hivyo inasaidia kupunguza ama kumaliza kabisa ajali za 
barabarani huku akifafanua Serikali itaendelea kuweka alama za usalama 
barabarani ili kuondoa changamoto za ajali.Amesema
 kuwa kutokea kwa elimu hiyo kwa Jiji la Dodoma kunakwenda kutengeneza 
jamii yenye mabalozi wazuri katika kutoa elimu ya usalama barabarani 
huku akieleza Dodoma ni ya pili kwa mtandao wa barabara za lamo,hivyo ni
 muhimu elimu hiyo kuendelea kutolewa.
"Nimesikia
 ombi la walimu na wanafunzi la kuhitaji alama za barabarani, hivyo 
Serikali itaendelea kuweka alama hizo.Pia nimezungumza na wenzetu wa 
Puma wamekubali kupaka rangi za usalama barabarani na wataanza na shule 
tano ambazo zimepatiwa elimu hii ya usalama barabarani,"amesema Mavunde
Wakati
 huo huo walimu wakuu katika shule za msingi katika Jiji la Dodoma 
wametoa ombi la kuweka alama za barabarani na hasa alama za pundamilia 
au matuta ili kuhakikisha wanafunzi wanapovuka wanakuwa salama kwani 
barabara nyingi hazina alama hizo.
Mwalimu
 Mkuu wa Shule ya Msingi General Musuguri Beatrice Chidumizi amesema 
changamoto iliyopo kwenye eneo la shule yao ni kukosekana kwa matuta au 
alama za barabarani, hivyo wanalazimika kumuweka mtu wa kuvusha 
wanafunzi ambaye analipwa fedha.
"Changamoto
 kubwa iliyopo katika shule yetu ni barabara yetu kutokuwa na matuta na 
alama za pundamilia,hivyo tunaomba tuwekewe alama za barabarani kwa 
ajili ya usalama wa wanafunzi wetu.Tunaishukuru Puma kwani imetusaidia 
sana kuwajengea uelewa wanafunzi wetu na sasa wanafahamu cha kufanya 
wanaoutaka kuvuka barabara.
"Tunaamini
 kupitia mafunzo haya tutapunguza ajali kwa watoto wetu na watumiaji 
wengine wa barabara zetu,"alisema Mwalimu Chidumizi na kuongeza kuwa 
umefika wakati kwa elimu hiyo kuendelea kutokea kwa Jiji la Dodoma hasa 
kwa kuzingatia Dodoma inakuwa kwa kasi kutokana na Serikali kuhamia 
Dodoma.


No comments:
Post a Comment