HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 10, 2019

Balozi Seif kuwaongezea muda madaktari wageni

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwakaribisha Zanzibar Madaktari Mabingwa Wapya na kuwaaga wale waliomaliza Muda wao Mwaka Mmoja wa kutoa huduma za Afya wanaotoka Nchini Jamuhuri ya Watu wa China.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara wa Afya Zanzibar Bibi Halima Salum Maulid akifafanua mafanikio ya huduma za Afya kutokana na uwepo wa Madaktari mabingwa kutoka China.
 Balozi Seif akipokea zawadi kutoka kwa Kiongozi wa Madaktari Mabingwa kutoka Jauhuri ya Watu wa China waliomaliza Muda wao hapa Zanzibar Dr. Zhang Zhen
 Balozi Seif kati kati waliokaa vitini katika katika picha ya pamoja na Madaktari Mabingwa Wapya na kuwaaga wale waliomaliza Muda wao Mwaka Mmoja wa kutoa huduma za Afya wanaotoka Nchini Jamuhuri ya Watu wa China.
Timu ya Madaktari Mabingwa Wapya na kuwaaga wale waliomaliza Muda wao wa China wakiagana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif mara baada ya kumaliza mazungumzo yao. Picha na – OMPR – ZNZ.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatafakari kuangalia uwezekano wa kuiomba Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China kuwaongezea muda wa kutoa huduma za Afya Madaktari wa Nchi hiyo wanaopangiwa kufanyakazi katika Hospitali za Rufaa hapa Zanzibar.

Alisema kutokana na ukarimu na huduma bora za Madaktari hao wanazozitoa kwa Wananchi upo umuhimu wa kuombewa muda wa Miaka Miwili badala ya ule Mmoja uliozoeleka katika Mkataba uliosainiwa kati ya Serikali hizo mbili mnamo Mwaka 1965.

Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar wakati akiwakaribisha Zanzibar Madaktari Mabingwa Wapya na kuwaaga wale waliomaliza Muda wao Mwaka Mmoja wa kutoa huduma za Afya kutoka Nchini Jamuhuri ya Watu wa China.

Alisema Jamii ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla tayari wanazikubali huduma zinazotolewa na Madaktari Bingwa kutoka Nchini China kiasi kwamba uwepo wao katika kipindn cha Mwaka Mmoja kinaonyesha kutokidhi kiu na mahitaji halisi ya Wananchi hao katika kupata huduma hiyo.

Alisema licha ya mazingira ya kupendeza kuona Madaktari wakongwe wanaondoka na wapya wanaingia kwa wakati katika kutoa matibabu ya Maradhi mbali mbali lakini bado muda wa ziada kwa mabingwa hao unahitajikja kwa vile tayari wameshakuwa kama Wana Jamii.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliishukuru na kuipongeza Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China kwa moyo wake wa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika Sekta ya Afya.

Mapema Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Hamad Rashid Mohamed alisema iliyoingia Nchini hivi sasa ni Timu ya 29 ya Madaktari Mabingwa wa China ikiwa ni mfumo maalum ulioasisiwa tokea Mwaka 1965 wa kuwapokea Wataalamu hao kwa lengo la kutoa huduma za Afya Zanzibar.

Mh. Hamad alisema Timu ya Madaktari ya Awamu ya 28 ilifanya kazi kubwa kama zilivyofanywa zile zilizotanguliwa kazi ambayo inastahiki kuendelezwa na Timu Mpya iliyoingia Nchini kushika dhamana hiyo.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Madaktari Mabingwa wa China waliomaliza Muda wao Kiongozi wa Madaktari hao Dr. Zhang Zhen alisema Timu hiyo imefanya kazi kubwa iliyoelata mafanikio makubwa kutokana na ushirikiano walioupata kutoka kwa Madaktari Wazawa.

Dr. Zhang alisema katika utumishi wao wa Mwaka Mmoja waliokuwepo Zanzibar Mabingwa hao wameweza kukabiliana na kesi 100 zilizokuwa zikiwasumbua Wananchi na kuzipatia ufumbuzi wa Kitaaluma.

Alisema Mabingwa hao waliomaliza muda wao walikuwa na mpango Maalum uliowawezesha kutoa huduma za Afya katika Hospitali mbali mbali za Mikoa, Wilaya hadi Vijijini.

Alifahamisha kwamba huduma hizo zilikwenda sambamba na utolewaji wa mafunzo kwa Madaktari Wazalendo pamoja na Semina zilizoshirikisha Watendaji wa Afya pamoja na wale wanaohusika na utoaji wa huduma ya kwanza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad