HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 12, 2019

NEMC kuingia mtaani kuangalia vvifungashio kutumika vibebesheo

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Baraza la Uhifadhi na Usimamizi  wa Mazingira (NEMC)  limepiga marufuku matumizi  ya vifungashio  vinavyotumika kuwa vibebesheo vya bidhaa mbalimbali.

Akizungumza na waandishi  wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Samuel Gwamaka amesema vifungashio vimeingia kwa kasi kutumika kwa ajili ya kubebea bidhaa mbalimbali ambapo hakuna tofauti  na mifuko ya plastiki ya Rambo na Mifuko laini Soft (Rambo).

Amesema kuwa NEMC inaingia mtaani kwa nchi nzima kuangalia mifuko hiyo na atakayekutwa na mifuko hiyo ashike faini ya sh.30,000 na kuendelea.
"Serikali  imepiga marufuku mifuko ya plastiki  hivyo hakuna njia mbadala ya kutumia mifuko hiyo plastiki  kwa kudai mifuko  ya vifungashio imeruhusiwa"amesema Gwamaka. 

Gwamaka  amesema watu wakiingia  mtaani mifuko  yeyote ile  kwani mifuko mbadala ipo lakini mingine ina ghafi ya plastiki  itaondolewa katika soko. Aidha amesema kuwa wananchi watoe ushirikiano  ikiwa ni kuacha kutumia mifuko ya plastiki wanayodai vifungashio.
 Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt Samuel Gwamaka akizungumza na waandishi habari  kuhusiana na watumiaji wa vifungashio vinavyotumika Kama vibebesheo ambapo ni kosa kisheria iliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt Samuel Gwamaka akionesha vifungashio kutumika kama vibebesheo

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad