HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, May 22, 2019

COSTECH yaendesha mafunzo kwa wadau katika utafiti

 Mafunzo ya Siku mbili ambayo yameandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia yamefugwa rasmi June 21 mwaka huu Mkoani Mtwara ambayo yalikuwakutanisha Watafiti,Waandishi Wa Habari na Wataalam kutoka taasisi mbalimbali  za utafiti kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara zikiwemo VETA na SIDO pamoja  Taasisi za elimu ya juu na kilimo.

Akifunga Mafunzo hayo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Tume hiyo Dr Bakari Msangi amewapongeza washiriki kwa Kuhudhuria na kuwataka kuyafanyia kazi yale waliyojifunza ili ilete tija kwa Jamii Husika 

Dr.Msangi amesema pia kazi ya Tume ni kuratibu na kushauri hivyo amewaomba Watafiti kutoa matokeo ya Utafiti wao nje na njia bora ni kwa kuwatumia Wanahabari Kama daraja kwa Jamii

Kwa upande mwingine ameahidi kuwatunikia vyeti vilivyosainiwa nakurugenzi Mkuu wahitimu wote Wa Mafunzo Kama sehemu ya kutambua na kuthamini mchango wao 

Kwa upande wake Afisa Habari Wa Mkoa Wa Mtwara Bw.Evarist Masuha ameishukuru COSTECH na kuwaomba kushirikiana na Mkoa katika mambo mbalimbali yanayohusu Sayansi teknolojia na Ubunifu.
 Mwakilishi wa mkurugenzi mkuu wa Tume ya Taifa ya sayansi na Teknolojia COSTECH Dkt.Bakari Msangi  (katikati) akifunga mafunzo ya siku  mbili ambayo yaliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia yamefugwa rasmi June 21 mwaka huu Mkoani Mtwara ambayo yalikuwakutanisha Watafiti,Waandishi Wa Habari na Wataalam kutoka taasisi mbalimbali  za utafiti kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara zikiwemo VETA na SIDO pamoja  Taasisi za elimu ya juu na kilimo.
 Afisa habari mkoa wa Mtwara akiishukuru COSTECH kwa kuona umuhimu wa kuleta mafunzo mkoani Mtwara 
Baadhi ya washiriki katika mafunzo ya siku  mbili ambayo yaliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia yamefugwa rasmi June 21 mwaka huu Mkoani Mtwara ambayo yalikuwakutanisha Watafiti,Waandishi Wa Habari na Wataalam kutoka taasisi mbalimbali  za utafiti kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara zikiwemo VETA na SIDO pamoja  Taasisi za elimu ya juu na kilimo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad