HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 19, 2019

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI LA MRADI WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA WA MJI WA MISUNGWI

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa   (kulia) wakimsikiliza, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji  na Usafi wa Mazingira  Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi Anthony Sanga (kushoto) alipotoa maelezo kuhusu ujenzi wa Mradi wa Maji na Usafi  wa Mazingira  wa Mji wa Misungwi katika kijiji cha Nyahiti Mkoani Mwanza, Machi 19, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa  Mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa Mji  wa Misungwi katika kijiji cha Nyahiti mkoani Mwanza, Machi 19, 2019. Kushoto  kwake ni Waziri wa Maji, Profesa, Makame Mbarawa na  kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira  Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi Anthony Sanga kuhusu michoro ya Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira  wa Mji wa Misungwi kabla ya kuweka jiwe la msingi la Mradi huo, Machi 19, 2019.  Wa pili kulia ni Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa, kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella na wa pili kushoto ni  Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua mashine za  za kusukuma maji kabla ya kuweka jiwe la msingi la  Mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira wa  Mji wa Misungwi katika kijiji cha Nyahiti mkoani Mwanza, Machi 19, 2019. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipongezwa na Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Mradi wa Maji  na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Misungwi katika kijiji cha Nyahiti Mkoani Mwanza, Machi 19, 2019.  Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mwanza, Anthony Daallo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad