Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na wananchi wa
Kilosa, Mkoani Morogoro, jana, ambapo amewaagiza Makamanda wa Polisi
nchini kuwachunguza na kuwakamata wapinzani wanaomtukana Rais pamoja na
Serikali kwa ujumla kupitia vikao vyao vya ndani vya siasa, nchini.
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akimsalimia Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kilosa, Amer Mbaraka, wakati alipokuwa anawasili katika Mkutano wa hadhara, mjini humo, Mkoani Morogoro, jana, kwa ajili ya kuzungumza na wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya Wizara yake. Katikati ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Adam Mgoyi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akimsalimia Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kilosa, Amer Mbaraka, wakati alipokuwa anawasili katika Mkutano wa hadhara, mjini humo, Mkoani Morogoro, jana, kwa ajili ya kuzungumza na wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya Wizara yake. Katikati ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Adam Mgoyi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akimfafanulia jambo
Mkazi wa Mji wa Kimamba, Wilayani Kilosa, Aris Diamond, wakati alipokuja
kutoa kero yake, katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini humo,
jana. Lugola aliwataka Polisi Mkoani Morogoro kufuata sheria na
utaratibu uliopangwa na Jeshi la Polisi bila kuwanyanyasa wananchi
wakati taarifa za malalamiko ya ardhi yanaporipotiwa vituoni. Picha na
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkazi wa Mji wa Kilosa, Mkoani Morogoro, Juma Haruni akitoa malalamiko yake ya ardhi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (hayupo pichani), wakati wa mkutano wa hadhara ulioitishwa na Waziri huyo, na kufanyika katika uwanja wa Kilosa Town, Mkoani Morogoro, jana. Lugola aliwataka Polisi Mkoani Morogoro kufuata sheria na utaratibu uliopangwa na Jeshi la Polisi bila kuwanyanyasa wananchi wakati taarifa za malalamiko ya ardhi yanaporipotiwa vituoni. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkazi wa Mji wa Kilosa, Mkoani Morogoro, Juma Haruni akitoa malalamiko yake ya ardhi kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (hayupo pichani), wakati wa mkutano wa hadhara ulioitishwa na Waziri huyo, na kufanyika katika uwanja wa Kilosa Town, Mkoani Morogoro, jana. Lugola aliwataka Polisi Mkoani Morogoro kufuata sheria na utaratibu uliopangwa na Jeshi la Polisi bila kuwanyanyasa wananchi wakati taarifa za malalamiko ya ardhi yanaporipotiwa vituoni. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
No comments:
Post a Comment