HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 12, 2019

WAZIRI JAFO ACHUKIZWA NA WATUMISHI WAZEMBE AMBAO WANASHINDWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO

WAZIRI wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo amechukizwa kuona baadhi ya viongozi na watendaji kutotimiza majukumu yao ipasavyo ikiwemo kufanya mambo kienyeji kwa kupokea miradi ya maendeleo pasipo kufahamu mwenendo mzima wa mkataba ulivyo pamoja na kutojua gharama za  fedha ambazo zinatolewa kwa ajili ya utekelezaji.

Jafo ametoa kauli hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kituo cha afya cha mlandizi kilichopo Wilayani Kibaha mkoani Pwani kwa lengo la kujieneo mwenendo mzima wa ukarabati wa majengo pamoja na kujionea ujenzi wa majengo matatu ambayo yamejengwa kwa kiasi cha shilingi milioni 400 fedha ambazo zimetolewa na serikali kuu.

Pia Jafo alibainisha kuwa hawezi kuwavumilia watumishi ambao ni wazembe na wanashindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo na kuwataka kuachana mara moja na vitendo vya kujihusiha na ubadhilifu wa fedha ambazo zinatolewa na serikali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo.

 “Mimi kama  kiongozi wetu sipendi kuona kabisa mnafanya kazi kienyeji bila ya kuzingatia sheria na taratibu amabzo zimewekwa na nchi, na katika hili siwezi kulifumbia macho maana maeneo mengine nimepita nimekuta miradi mingine bado inasua sua nah ii ni baadhi ya watu kutotimiza majukumu yao ipasavyo ni ninachotaka miradi yote inapokuja lazima wahusika kufahamu mikatab ailivyo pamoja na fedha ambayo inatolewa sio kupokea tu,”alisema Jafo.

Aidha aliseama kwamba serikali ya awamu ya tano kwa sasa imeshatoa fedha katika vituo vya afya  zaidi ya 90 hapa nchini   kwa lengo la kuweza kuongeza majengo mengine pamoja na kufanya ukarabati wa miundombinu ya wodi mbali mbali ikiwemo nyumba za watumishi kwa lengo la kuweza kuboresha sekta ya afya kwa wananchi.

Aidha katika hatua nyingine Jafo ameupongeza uongozi wa halmashauri ya Kibaha vijijini  kwa kutekeleza agizo lake la kukukarabati  chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha afya mlandizi ambapo hapo awali kilikuwa hakifanya kazi kabisa kwani kiligeuzwa kuwa  eneo la stoo na kuhifadhia vyuma chakavu.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Kibaha vijijini  Butamo  Nuru alisema  kwamba wametekeleza agizo ambalo walipatiwa na waziri wa Tamisemi la kukarabati miundombinu ya chumba cha kuhifadhia maiti pamoja na kununua majokofu  nane ambayo yamegharimi kiasi cha shilingi milioni 36.

WAZIRI Jafo katika ziara yake ya kikazi kwa  halmashauri ya Kibaha vijijini ameweza kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa  majengo matatu ya wodi ya upasuaji,wazazi,na wagonjwa wa nje (OPD) sambamba na kutembelea miradi mingine miwili ya ujenzi wa hospotali pamoja na jengo la  ofisi za halmashauri hiyo.
 Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za miko na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo kushoto akimpa maelekezo Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama wa kulia kuhusiana na usimamiza wa fedha zinazotolewa katika miradi mbalimbali ya maendeleo katikati ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Homoud Jumaa mara baada ya kukagua ujenzi wa wodi tatu zilizojengwa katika kituo cha afya mlandizi  pamoja na kujionea ukarabati wa  chumba cha kuhifadhia maiti.
 Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za miko na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo kushoto akimpa maelekezo Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama wa kulia kuhusiana na usimamiza wa fedha zinazotolewa katika miradi mbalimbali ya maendeleo katikati ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Homoud Jumaa mara baada ya kukagua ujenzi wa wodi tatu zilizojengwa katika kituo cha afya mlandizi  pamoja na kujionea ukarabati wa  chumba cha kuhifadhia maiti.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za miko na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo kushoto akimpa maelekezo Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama wa kulia kuhusiana na usimamiza wa fedha zinazotolewa katika miradi mbalimbali ya maendeleo katikati ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Homoud Jumaa mara baada ya kukagua ujenzi wa wodi tatu zilizojengwa katika kituo cha afya mlandizi  pamoja na kujionea ukarabati wa  chumba cha kuhifadhia maiti.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad