HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, March 30, 2019

Serikali yaiagiza BMT Kuhakikisha Uchaguzi ndani ya Klabu ya Yanga unafanyika ndani ya Siku 30

 Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari utamaduni Sanaa na Michezo Bw.Yusuph Singo (Kushoto) akizungumza na Waandishi wa Habari leo Machi 30, 2019 Jijini Dodoma kuhusu kuliagiza Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kusimamia Uchaguzi ndani ya Klabu ya Dar es Salaam Young Africans (Yanga) ufanyike ndani ya siku 30 kuanzia leo.Kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Bw.Alex Nkenyenge.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa Bw.Alex Nkenyenge (Kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari leo Machi 30, 2019 Jijini Dodoma kuhusu kutekeleza maagizo ya Serikali kwa  Baraza hilo kusimamia Uchaguzi ndani ya Klabu ya Dar es Salaam Young Africans (Yanga) ndani ya siku 30 kuanzia leo.Kushoto ni Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari utamaduni Sanaa na Michezo Bw.Yusuph Singo.

Na Shamimu nyaki –WHUSM
Serikali imeliagiza Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kushirikiana na Shirikisho la mpira wa Miguu (TFF) kuhakikisha uchaguzi ndani ya Klabu ya Dar es Salaam Young Africans (Yanga) unafanyika ndani ya siku 30 kuanzia leo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw.Yusuph Singo katika mkutano na Waandishi wa Habari leo Jijini Dodoma ambapo amesema kuwa migogoro iliyokuwepo huko nyuma imeshafika tamati hivyo uchaguzi ndani ya Klabu hiyo ni lazima ufanyike.
“Nailekeza BMT iwaelekeze TFF kuhakikisha taratibu zote za uchaguzi zinafuatwa na uchaguzi ndani ya Klabu ya Dar es Salaam Young Africans unafayika ndani ya siku 30 kuanzia sasa”.alisema Bw.Singo
Aidha Bw.Singo amewahisi Viongozi, wanachama na wapenzi wa Klabu ya Dar es Salaam Young Africans kutoanzisha migogoro wala vikwazo vingine bali kutumia siku 30 hizo kufanya uchaguzi ili kupata viongozi watakaoisimamia na kuiongoza Klabu hiyo kuendelea kufanya vizuri katika mpira wa miguu ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bw.Alex Nkenyenge amesema amepokea maagizo na atayafanyia kazi mara moja ili kipindi kilichowekwa na Serikali cha siku 30 Klabu ya Yanga iwe tayari ina uongozi.
Bw.Nkenyenge ameongeza kuwa atahakikisha Kamati ya Uchaguzi ya TFF inapanga utaratibu unaotakiwa kufuatwa kulingana na Katiba ya Shirikisho hilo ili Uchaguzi huo ufanyike hatimaye migogoro iliyodumu kwa muda mrefu ndani ya Klabu hiyo ifikie mwisho na Klabu iendelee kufanya vizuri katika mpira wa miguu.
Klabu ya Dar es Salaam Young Africans (Yanga) ni miongoni mwa Klabu kubwa za mpira wa miguu hapa nchini ambayo kwa muda mrefu haijatekekeleza uchaguzi kwa mujibu wa Katiba yao.
……MWISHO……


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad