HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 21, 2019

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI MKAZI WA UN WOMEN

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa  linaloshughulikia Masuala ya Wanawake (UN-Women) Hodan Addou aliyeambatana na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Alvaro Rodriguez, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine Mwakilishi huyo wa UN-Women alizungumzia kazi mbalimbali zinazofanywa na Shirika hilo hapa nchini hususani katika kushirikiana na Serikali katika miradi mbalimbali ikiwemo Mkakati wa Kukuza Uchumi na kupumguza Umasikini Tanzania(MKUKUTA) na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar (MKUZA).
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan (kulia) akisalimia na Hodan Addou, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja  wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN-Women), mwingine pichani ni Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Alvaro Rodriguez ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan (kulia) akizungumza na Hodan Addou, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja  wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN-Women), pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa  Alvaro Rodriguez (katikati) ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais). 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na  Hodan Addou, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja  wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN-Women),pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Alvaro Rodriguez (kushoto) ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan (kulia) akitwa kwenye picha ya pamoja na Hodan Addou, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja  wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN-Women), mara baada ya kumaliza mazungumzo leo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan (kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa  Alvaro Rodriguez mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad