HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 26, 2019

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA NBC

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan leo tarehe 26, Machi 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo amefika ofisini kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kujitambulisha akiwa ameongozana na Meneja mahusiano na Serikali William Kalaghe pamoja na Afisa Masoko wa NBC Bi. Neemarose Singo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi (kushoto) ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi, Afisa  Masoko wa NBC Bi. Neenarose Singo pamoja na Meneja wa Mahusiano na Serikali Ndugu William Kallaghe (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja  na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi (kushoto) mara baada ya mazungumzo ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad