HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 14, 2019

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AFANYA ZIARA WILAYA YA MAGHARIBI B UNGUJA

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Daktari Dhamana wa Manispa ya Wilaya ya Magharibi B,Unguja Dkt. Rahma Abdallah Maisara, akitowa maelezo ya michoro ya jengo la Kituo cha Afya Magirisi Jimbo la Kijitoupele Zanzibar ,wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi, akiwa katika ziara yake katika Wilaya ya Magharibi Unguja leo.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubiua Wananchi wa Jimbo la Kijitoupele Zanzibar, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Kituo cha Afya cha Magirisi leo akiendelea na ziara yake katika Wilaya ya Magharibi B Unguja leo.
  BAADHI ya Wananchi na Viongozi wa Vyama vya Siasa wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, wakati akihutubia hafla hiyo ya uwekaji wa Jiwe la Msingi katika Kituo cha Afya cha Magirisi Jimbo la Kijitoupele Zanzibar, akiwa katika ziara yake ya Wilaya ya Magharibi B, Unguja kutembelea Miradi ya Maendeleo.
 MKURUGENZI wa Manispa ya Magharibi B, Unguja Ndg. Ali Abdallah Said Natepe, akitowa Taarifa ya Kitaalam ya Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Magirisi Wilaya ya Magharibi B, Unguja wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi leo ,wakati wa ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa katika ziara yake katika Wilaya ya Magharibi B,Unguja leo.
 WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.Mhe. Haji Omar Kheri, akizunguza katika hafla hiyo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, kuhutubia hafla hiyo katika viwanja vya Kituo cha Afya Magirisi Wilaya ya Magharib B, Unguja leo.
 MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa Chama kulia Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dr. Abdallah Juma Mabodi, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Magharibi Unguja Ndg. Mohammed Rajab Soun na kushoto Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maghjaribi Ndg Hussein Mjema (Kimti ), na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, wakiwa wamesimama wakati wakiimba wimbo wa Sisi Sote Tumekomboka,wakiwa katika ukumbi wa Afisi ya CCM Mkoa wa Mjini Amani Zanzibar, kuzungumza na Wanachama wa CCM Wilaya ya Magharibi Unguja.
 MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wanachama wa CCM wa Mkoa wa Magharibi Kichama, uliuofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Afisi ya CCM Mkoa wa Mjini Unguja, akiwa katika ziara yake katika Wilaya ya Magharibi B, Unguja iliofanyika leo,14-2-2019.
 KATIBU wa CCM Wilaya ya Dimani Unguja Ndg.Yussuf Ramadhan Abdallah akisoma Ripoti ya Utekelezaji wa CCM ya Wilaya, wakati wa hafla ya Mkutano na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein,uliofanyika katika ukumbi wa Afisi ya CCM Mkoa wa Mjini Amani Unguja  leo.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dr. Abdallah Juma Mabodi akizungumza wakati wa Mkutano wa ndani wa CCM wakati wa ziara ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, kuzungumza na Wanachama wa CCM wa Mkoa wa Magharibi Unguja, uliofanyika katika ukumbi wa CCM Amani Mkoa.
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Magharibi Kichama Ndg. Mohammed Rajab Soud, akizungumza na kutowa shukrani za Mkoa wake kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar.Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad