HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 8, 2019

MAKATIBU WAKUU WA TANZANIA BARA NA ZANZIBAR WAKUTANA KUJADILIANA MASUALA YA MUUNGANO

 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Joseph Malongo (kushoto) akiendesha kikao kazi cha Makatibu Wakuu kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Pamoja na mambo mengine kikao hicho kimejadili juu ya uratibu na ufuatiliaji wa masuala ya Muungano.  Kulia ni Bw. Abdallah Mitawi Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ambae ni Mwenyekiti Mwenza. Kikao hicho kimefanyika hii leo katika Ukumbi wa Hazina, Jijini Dodoma.
 Sehemu ya Wajumbe wa kikao hicho ambao ni Makatibu Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) wakifuatilia kikao hicho. Jumla ya Makatibu Wakuu 26 kutoka Tanzania Bara wamehudhuria kikao hicho.
Sehemu ya Wajumbe wa kikao hicho ambao ni Makatibu Wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) wakifuatilia kikao hicho, kilichofanyika katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma. Jumla ya Makatibu Wakuu 13 kutoka Zanzibar wamehudhuria ikiwa ni maandalizi ya kikao cha Kamati ya pamoja kitakachofanyika siku ya kesho Mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad